Skip to Content
The Muslims Internet Directory
Featured Service
Home
|
Advertise
|
FAQ
|
Login/Register |
Directory
Quran
Hadith
Islamic Library
Prayer Times
Discover Islam
Islamic Gallery
Calendar
New
Classifieds
Services
Webmasters
Dictionary
Downloads
Kids & Games
Quran Navigation
Search
Translations
Transliteration
Index
Chapter Info
English Search
Articles and Books
Audio
Memorization
Links
Downloads
On Your Site
FAQ
Muslims Internet Directory
The Quran / English
The Hadith
2Muslims.com
Our Network
Islamic Library & Articles
The Internet
Islamic Classifieds
WebRing Members Sites
Advance
-
Live Search
-
Quran
-
Hadith
-
Search This Site
-
The Network
-
Classifieds
-
WebRing
-
The Internet
-
Help!
Featured Site
Feature Your Site Now
2Muslims Services
Islamic IE Toolbar
Islamic Internet Gadgets
Prayer Times Software
Forum
Donate
Islamic Quizzes
Islamic CGI Scripts
Polls
Free E-mail Account
Zakat Calculator
Islamic Holidays Dates
Islamic Date Converter
DAWA Tools
FAQ About Islam
Buy The Islamic CD
God's Attributes
How To Pray?
Paid Services
Buy The Islamic CD
Banner Design
Submit Your Site
Muslims Million Pixels
Translate Site To:
Arabic
Bulgarian
Catalan
Chinese (Simplified)
Chinese (Traditional)
Croatian
Czech
Danish
Dutch
English
Filipino
Finnish
French
German
Greek
Hebrew
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latvian
Lithuanian
Norwegian
Polish
Portuguese
Romanian
Russian
Serbian
Slovak
Slovenian
Spanish
Swedish
Ukrainian
Vietnamese
Hijab
Why do muslim females wear Hijab (Head cover)?
Faith
Culture
Fear
Other
view results
view other polls
Home
:
Quran:
Quran Translations:
Swahili:
SURAT IBRAHIM :
Search the Quran in any of the drop down menu languages:
--Select language--
Albanian
Arabic
Azerbaijani
Bengali
Bosnian
Brazilian
Burmese
Chinese
Dutch
English_Abdullah_Yusuufali
English_Hasan_Qaribullah
English_Muhammad_Pickthall
Farsi
Finish
French
German
Hausa
Hindi
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latin
Malaysian
Melayu
Meranao
Mexican
Pashto
Persian
Poland
Portuguese
Russian
Spanish
Swahili
Tamil
Thai
Transliteration
Turkish
Urdu
More search options
SURAT IBRAHIM
[14.1] Alif Lam Ra. (A.L.R.) Hichi ni Kitabu tulichokiteremsha kwako ili uwatowe watu kwenye gizauwapeleke kwenye muwangaza, kwa idhini ya Mola waoMlezi, uwafikishe kwenye Njia ya Mwenye nguvu,Msifiwa,
[14.2] Naye ni Mwenyezi Mungu ambaye ni vyake Yeye vyoteviliomo katika mbingu na ardhi. Na ole wao makafirikwa adhabu kali!
[14.3] Wale wanao fadhilisha maisha ya dunia kulikoAkhera, na wanawazuilia watu wasifuate Njia yaMwenyezi Mungu, na wanataka kuipotosha. Haowamepotelea mbali.
[14.4] Na hatukumtuma Mtume ila kwa ulimi wa kaumu yakeili apate kuwabainishia. Basi Mwenyezi Mungu humuachaakapotea amtakaye, na akamwongoa amtakaye. Naye ni Mtukufu Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
[14.5] Na tulimtuma Musa pamoja na miujiza yetu,tukamwambia: Watoe watu wako kwenye giza uwapelekekwenye mwangaza. Na uwakumbushe siku za MwenyeziMungu. Hakika katika hayo zipo ishara kwa kila mwenyekusubiri akashukuru.
[14.6] Na Musa alipo waambia watu wake: Kumbukeni neema yaMwenyezi Mungu aliyo kujaalieni, pale alipo kuokoenikutokana na watu wa Firauni walio kupeni adhabu mbaya kabisa, wakiwachinja wenenu wanaume, nawakiwawacha hai wanawake. Na katika hayo ulikuwamtihani mkubwa unao toka kwa Mola wenu Mlezi.
[14.7] Na alipo tangaza Mola wenu Mlezi: Mkishukurunitakuzidishieni; na mkikufuru, basi adhabu yangu nikali.
[14.8] Na Musa alisema: Mkikufuru nyinyi na wote waliomoduniani, hakika Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Anajitosha,Msifiwa.
[14.9] Je! Hazikukufikieni khabari za walio kabla yenu?Kaumu ya Nuhu, na A'adi, na Thamud, na walio baadayao, ambao hapana awajuaye ila Mwenyezi Mungu? Mitumewao waliwajia kwa hoja zilizo wazi, na wao wakarudishamikono yao kwenye vinywa vyao, wakasema: Hakika sisitumeyakataa hayo mliyo tumwa, na hakika sisi tuna shaka kubwa na mnayo tuitia.
[14.10] Mitume wao wakasema: Ati pana shaka na MwenyeziMungu, Muumba mbingu na ardhi? Yeye anakuiteni apatekukufutieni madhambi yenu, na akupeni muhula mpaka muda ulio wekwa. Wakasema: Nyinyi si chochote ila niwanaadamu kama sisi. Mnataka kutuzuilia na waliyo kuwawakiabudu baba zetu. Basi tuleteeni hoja ilio wazi.
[14.11] Mitume wao wakawaambia: Sisi kweli si chochote ilani wanaadamu kama nyinyi. Lakini Mwenyezi Munguhumfanyia hisani amtakaye katika waja wake. Wala sisi hatuwezi kuleta uthibitisho ila kwa idhini ya MwenyeziMungu. Na juu ya Mwenyezi Mungu ndio wategemeeWaumini.
[14.12] Na tuna nini hata tusimtegemee Mwenyezi Mungu, nahali Yeye ametuongoa kwenye Njia zetu. Na hapana shakasisi tutayavumilia hayo maudhi mnayo tuudhi. Na juu ya Mwenyezi Mungu wategemee wanao tegemea.
[14.13] Na walio kufuru wakawaambia Mitume wao:Tutakutoeni katika nchi yetu, au mrudi katika milayetu. Basi Mola wao Mlezi aliwaletea wahyi: Hakika tutawaangamiza walio dhulumu!
[14.14] Na tutakuwekeni katika ardhi baada yao. Haya nikwa anaye ogopa kusimamishwa mbele yangu, na akaogopamaonyo yangu.
[14.15] Na wakaomba ushindi, na akashindwa kila jabarimkaidi,
[14.16] Ambaye nyuma yake ipo Jahannamu, na atanywishwamaji ya usaha.
[14.17] Awe anayagugumia, wala hawezi kuyameza. Na mautiyawe yanamjia kutoka kila upande, naye wala hafi. Nazaidi ya hayo ipo adhabu nyengine kali vile vile.
[14.18] Mfano wa walio mkufuru Mola wao Mlezi - vitendovyao ni kama jivu linalo peperushwa kwa nguvu za upepokatika siku ya mdharba. Hawawezi kupata chochote katika waliyo yafanya. Huko ndiko kupotelea mbali!
[14.19] Huoni kuwa Mwenyezi Mungu ameziumba mbingu naardhi kwa Haki? Akitaka atakuondoeni na alete viumbewapya!
[14.20] Na hilo kwa Mwenyezi Mungu si jambo gumu.
[14.21] Na wote watahudhuria mbele ya Mwenyezi Mungu.Wanyonge watawaambia walio takabari: Sisi tulikuwawafwasi wenu; basi hebu hamtuondolei kidogo hivikatika adhabu ya Mwenyezi Mungu? Watasema: LauMwenyezi Mungu angeli tuongoa basi hapana shaka nasitungeli kuongoeni. Ni mamoja kwetu tukipapatika autukisubiri; hatuna pa kukimbilia.
[14.22] Na Shet'ani atasema itapo katwa hukumu: HakikaMwenyezi Mungu alikuahidini ahadi ya kweli. Naminalikuahidini; lakini sikukutimizieni. Na sikuwa namamlaka juu yenu, isipo kuwa nilikuiteni, nanyimkaniitikia. Basi msinilaumu mimi, bali jilaumuni wenyewe. Mimi siwezi kuwa mtetezi wenu, walanyinyi hamwezi kuwa watetezi wangu. Hakika miminilikataa tangu zamani kunishirikisha na Mwenyezi Mungu. Hakika madhaalimu watakuwa na adhabu chungu.
[14.23] Na walio amini na wakatenda mema wataingizwakatika Mabustani yapitayo mito kati yake, wadumu humokwa idhini ya Mola wao Mlezi. Maamkio yao humoyatakuwa: Salaam!
[14.24] Hebu hukuona vipi Mwenyezi Mungu alivyo piga mfanowa neno zuri? Ni kama mti mzuri, mizizi yake ni imara,na matawi yake yako mbinguni.
[14.25] Hutoa matunda yake kila wakati kwa idhini ya Molawake Mlezi. Na Mwenyezi Mungu huwapigia watu mifanoili wapate kukumbuka.
[14.26] Na mfano wa neno ovu ni kama mti muovu, uliong'olewa juu ya ardhi. Hauna imara.
[14.27] Mwenyezi Mungu huwatia imara wenye kuamini kwakauli ya imara katika maisha ya dunia na katikaAkhera. Na Mwenyezi Mungu huwaacha kupotea hao wenye kudhulumu. Na Mwenyezi Mungu hufanya apendavyo.
[14.28] Hebu hukuwaona wale walio badilisha neema yaMwenyezi Mungu kwa kufuru, na wakawafikisha watu waokwenye nyumba ya maangamizo?
[14.29] Nayo ni Jahannamu! Maovu yaliyoje makaazi hayo!
[14.30] Na walimfanyia Mwenyezi Mungu washirika iliwapoteze watu kwenye Njia yake. Sema: Stareheni! Kwanimarejeo yenu ni Motoni!
[14.31] Waambie waja wangu walio amini, washike Sala, nawatoe katika tulivyo waruzuku, kwa siri na dhaahiri,kabla haijafika Siku isiyo kuwa na biashara wala urafiki.
[14.32] Mwenyezi Mungu ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi,na akateremsha maji kutoka mbinguni. Na kwa hayoakatoa matunda kuwa ni riziki yenu. Na akafanya yakutumikieni majahazi yanayo pita baharini kwa amriyake, na akaifanya mito ikutumikieni.
[14.33] Na akalifanya jua na mwezi kwa manufaa yenu daimadawamu, na akaufanya usiku na mchana kwa manufaa yenu.
[14.34] Na akakupeni kila mlicho muomba. Na mkihisabuneema za Mwenyezi Mungu hamwezi kuzidhibiti. Hakikamwanaadamu ni dhaalimu mkubwa, mwenye kuzikufuru neema.
[14.35] Na Ibrahim alipo sema: Ewe Mola wangu Mlezi!Ujaalie mji huu uwe wa amani, na uniepushe mimi nawanangu na kuabudu masanamu.
[14.36] Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika hayo yamewapotezawatu wengi. Basi aliye nifuata mimi huyo ni wangu, naaliye niasi, hakika Wewe ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
[14.37] Mola wetu Mlezi! Hakika mimi nimewaweka baadhi yadhuriya zangu katika bonde lisilo kuwa na mimea,kwenye Nyumba yako Takatifu, ewe Mola wetu Mlezi, ili washike Sala. Basi zijaalie nyoyo za watu zielekeekwao, na waruzuku matunda, ili wapata kushukuru.
[14.38] Ewe Mola wetu Mlezi! Hakika Wewe unajua tunayoyaficha na tunayo yatangaza. Na hapana kitu kinachofichikana kwa Mwenyezi Mungu katika ardhi wala katika mbingu.
[14.39] Alhamdulillahi! Himdi zote ni za Mwenyezi Mungualiye nipa juu ya uzee wangu Ismail na Is-haq. HakikaMola wangu Mlezi ni Mwenye kusikia maombi.
[14.40] Mola wangu Mlezi! Nijaalie niwe mwenye kushikaSala, na katika dhuriya zangu pia. Ewe Mola wetuMlezi, na ipokee dua yangu.
[14.41] Mola wetu! Unighufirie mimi na wazazi wangu wotewawili, na Waumini, siku ya kusimama hisabu.
[14.42] Wala usidhani Mwenyezi Mungu ameghafilika nawanayo yafanya madhaalimu. Hakika Yeye anawaakhirishatu mpaka siku yatapo kodoka macho yao.
[14.43] Nao wako mbioni, vichwa juu, na macho hayapepesi,na nyoyo zao tupu.
[14.44] Na waonye watu siku itapo wajia adhabu, na waliodhulumu waseme: Ewe Mola wetu Mlezi! Tuakhirishe mudakidogo tuitikie wito wako na tuwafuate Mitume. Kwani nyinyi si mliapa zamani kwamba hamtaondokewa?
[14.45] Na mkakaa katika maskani zile zile za waliozidhulumu nafsi zao. Na ikakudhihirikieni jinsitulivyo watendea. Nasi tukakupigieni mifano mingi.
[14.46] Na kwa hakika walifanya vitimbi vyao, na vitimbivyao anavijua Mwenyezi Mungu. Wala vitimbi vyao si vyakuondosha milima.
[14.47] Basi usimdhanie Mwenyezi Mungu kuwa ni mwenyekuwavunjia ahadi yake Mitume wake. Hakika MwenyeziMungu ni Mwenye kushinda, na ni Mwenye kulipiza.
[14.48] Siku itapo geuzwa ardhi iwe ardhi nyengine, nambingu pia. Nao watahudhuria mbele ya Mwenyezi MunguMmoja, Mwenye nguvu.
[14.49] Na utaona wakhalifu siku hiyo wamefungwa katikaminyororo;
[14.50] Nguo zao zitakuwa za lami, na Moto utazigubikanyuso zao.
[14.51] Ili Mwenyezi Mungu ailipe kila nafsi kwa yaleiliyo yachuma. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wakuhisabu.
[14.52] Hili ni Tangazo liwafikie watu, liwaonye, nawapate kujua kuwa hakika Yeye ni Mungu Mmoja, nawapate kukumbuka wenye akili.
Featured Ad
About Us
Contact Us
Advertise
Donate
Bookmark Us
Support Us
GuestBook
Link To Us
Newsletter
Recommend
Set as Home
Terms Of Use
What's New
Other Sites:
Know The Prophet campaign
-
Discover Islam
-
Pharmacy Site
-
Links SQL Plugins
This Page Was Last Updated on
Copyright 2003-2008
Islamic Education & Services Institute