Skip to Content
The Muslims Internet Directory
Featured Service
Home
|
Advertise
|
FAQ
|
Login/Register |
Directory
Quran
Hadith
Islamic Library
Prayer Times
Discover Islam
Islamic Gallery
Calendar
New
Classifieds
Services
Webmasters
Dictionary
Downloads
Kids & Games
Quran Navigation
Search
Translations
Transliteration
Index
Chapter Info
English Search
Articles and Books
Audio
Memorization
Links
Downloads
On Your Site
FAQ
Muslims Internet Directory
The Quran / English
The Hadith
2Muslims.com
Our Network
Islamic Library & Articles
The Internet
Islamic Classifieds
WebRing Members Sites
Advance
-
Live Search
-
Quran
-
Hadith
-
Search This Site
-
The Network
-
Classifieds
-
WebRing
-
The Internet
-
Help!
Featured Site
Feature Your Site Now
2Muslims Services
Islamic IE Toolbar
Islamic Internet Gadgets
Prayer Times Software
Forum
Donate
Islamic Quizzes
Islamic CGI Scripts
Polls
Free E-mail Account
Zakat Calculator
Islamic Holidays Dates
Islamic Date Converter
DAWA Tools
FAQ About Islam
Buy The Islamic CD
God's Attributes
How To Pray?
Paid Services
Buy The Islamic CD
Banner Design
Submit Your Site
Muslims Million Pixels
Translate Site To:
Arabic
Bulgarian
Catalan
Chinese (Simplified)
Chinese (Traditional)
Croatian
Czech
Danish
Dutch
English
Filipino
Finnish
French
German
Greek
Hebrew
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latvian
Lithuanian
Norwegian
Polish
Portuguese
Romanian
Russian
Serbian
Slovak
Slovenian
Spanish
Swedish
Ukrainian
Vietnamese
Hijab
Why do muslim females wear Hijab (Head cover)?
Faith
Culture
Fear
Other
view results
view other polls
Home
:
Quran:
Quran Translations:
Swahili:
SURA AL KAHF :
Search the Quran in any of the drop down menu languages:
--Select language--
Albanian
Arabic
Azerbaijani
Bengali
Bosnian
Brazilian
Burmese
Chinese
Dutch
English_Abdullah_Yusuufali
English_Hasan_Qaribullah
English_Muhammad_Pickthall
Farsi
Finish
French
German
Hausa
Hindi
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latin
Malaysian
Melayu
Meranao
Mexican
Pashto
Persian
Poland
Portuguese
Russian
Spanish
Swahili
Tamil
Thai
Transliteration
Turkish
Urdu
More search options
SURA AL KAHF
[18.1] Kuhimidiwa ni kwa Mwenyezi Mungu, ambayeamemteremshia mja wake Kitabu, wala hakukifanya kinaupogo.
[18.2] Kimenyooka sawa, ili kitoe onyo kali kutoka kwake,na kiwabashirie Waumini watendao mema kwamba watapataujira mzuri.
[18.3] Wakae humo milele.
[18.4] Na kiwaonye wanao nena: Mwenyezi Mungu ana mwana.
[18.5] Wao hawana ujuzi wa jambo hili, wala baba zao. Nineno kuu hilo litokalo vinywani mwao. Hawasemi ilauwongo tu.
[18.6] Huenda ukajihiliki nafsi yako kwa ajili yao,kuwasikitikia kwa kuwa hawayaamini mazungumzo haya!
[18.7] Kwa hakika tumevifanya vilioko juu ya ardhi kuwa nipambo lake ili tuwafanyie mtihani, ni nani kati yaowenye vitendo vizuri zaidi.
[18.8] Na hakika Sisi tutavifanya vyote vilio juu ya ardhikuwa kama nchi ilio pigwa na ukame.
[18.9] Bali unadhani ya kwamba wale Watu wa Pangoni naMaandishi walikuwa ni ajabu miongoni mwa ishara zetu?
[18.10] Vijana hao walipo kimbilia kwenye pango walisema:Mola wetu Mlezi! Tupe rehema itokayo kwako, natutengezee uwongofu katika jambo letu.
[18.11] Tukayaziba masikio yao kuwalaza humo pangoni kwamuda wa miaka kadhaa wa kadhaa.
[18.12] Kisha tukawazindua ili tujue ni lipi katikamakundi mawili lilio hisabu sawa muda walio kaa.
[18.13] Sisi tunakusimulia khabari zao kwa kweli. Hakikawao walikuwa ni vijana walio muamini Mola wao Mlezi.Na Sisi tukawazidisha uwongofu.
[18.14] Na tukazitia nguvu nyoyo zao walipo simama nawakasema: Mola wetu Mlezi ni Mola Mlezi wa mbingu naardhi. Hatutamwita mwenginewe kabisa badala yake kuwani Mungu. Hivyo itakuwa tumesema jambo la kuvukampaka.
[18.15] Hawa watu wetu wameshika miungu mingine badalayake Yeye. Kwa nini basi hawawatolei uthibitisho uliodhaahiri? Na nani aliye dhaalimu zaidi kuliko anaye mzulia uwongo Mwenyezi Mungu?
[18.16] Na mkijitenga nao na vile wanavyo viabudu badalaya Mwenyezi Mungu, basi kimbilieni pangoni,akufungulieni Mola wenu Mlezi rehema yake, na akutengenezeeni ya kukufaeni katika mambo yenu.
[18.17] Na unaliona jua linapo chomoza linainamia kulianimwao kutoka hapo pangoni; na linapo kuchwa linawakwepakushotoni, na wao wamo katika uwazi wa pango. Hizo ni katika ishara za Mwenyezi Mungu. Ambaye MwenyeziMungu anamwongoa basi huyo ni mwenye kuongoka. Naanaye muacha kupotea basi hutampatia mlinzi wala mwongozi.
[18.18] Nawe utawadhania wamacho, na hali wamelala. Nasitunawageuza kulia na kushoto. Na mbwa wao amenyooshamiguu yake ya mbele kizingitini. Kama ungeli watokea hapana shaka ungeli geuka kuwakimbia, naweumejaa khofu.
[18.19] Na kwa namna hii tuliwainua usingizini wapatekuulizana wao kwa wao. Alisema msemaji katika wao:Mmekaa muda gani? Wakasema: Tumekaa siku moja ausehemu ya siku. Wakasema: Mola wenu Mlezi anajua zaidimuda mlio kaa. Hebu mtumeni mmoja wenu na hizi fedhazenu ende mjini, akatazame chakula chake kipi kilichobora kabisa akuleteeni cha kukila. Naye afanye mambohayo kwa busara, wala asikutajeni kabisa kwa yeyote.
[18.20] Kwani wao wakikutambueni watakupigeni mawe, auwatakurudisheni katika dini yao; na hapo hamtafanikiwakabisa!
[18.21] Na namna hivi tuliwa juulisha kwa watu wapatekujua ya kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ni ya kweli,na kwamba Saa haina shaka. Walipo kuwa wakigombania jambo lao wao kwa wao walisema: Jengeni jengo juu yao.Mola wao Mlezi anawajua vyema. Wakasema walio shindakatika shauri yao: Bila ya shaka tutawajengea msikiti juu yao.
[18.22] Watasema: Walikuwa watatu, wa nne wao ni mbwa wao.Na wanasema: Walikuwa watano, wa sita wao ni mbwa wao.Wanavurumisha ovyo. Na wanasema: Walikuwa saba, na wa nane wao ni mbwa wao. Sema: Mola wangu Mlezindiye anaye jua sawa sawa hisabu yao. Hawawajui ilawachache tu. Basi usibishane juu yao ila kwa mabishanoya juu juu tu hivi. Wala usiulize khabari zao kwayeyote yule.
[18.23] Wala usisema kamwe kwa jambo lolote lile: Hakikanitalifanya hilo kesho -
[18.24] Isipo kuwa Mwenyezi Mungu akipenda. Na mkumbukeMola wako Mlezi pale unapo sahau, na sema: Asaa Molawangu Mlezi ataniongoa kwenye uwongozi ulio karibu zaidi kuliko huu.
[18.25] Na walikaa katika pango lao miaka mia tatu, nawakazidisha tisa.
[18.26] Sema: Mwenyezi Mungu anajua zaidi muda walio kaa.Ni zake tu siri za mbingu na ardhi. Kuona kulioje nakusikia kwake! Hawana mlinzi isipo kuwa Yeye, wala hamshirikishi yeyote katika hukumu yake.
[18.27] Na soma uliyo funuliwa katika Kitabu cha Mola wakoMlezi. Hapana wa kubadilisha maneno yake. Wala nawehutapata makimbilio isipo kuwa kwake.
[18.28] Na isubirishe nafsi yako pamoja na wanao muombaMola wao Mlezi asubuhi na jioni, hali ya kuwa wanatakaradhi yake. Wala macho yako yasiwaruke kwa kutaka pambo la maisha ya dunia. Wala usimt'ii tuliyemghafilisha moyo wake asitukumbuke, na akafuatamatamanio yake yakawa yamepita mpaka.
[18.29] Na sema: Hii ni kweli itokayo kwa Mola wako Mlezi.Basi atakaye, aamini. Na atakaye, akatae. Hakika Sisitumewaandalia wenye kudhulumu Moto ambao utawazunguka kama khema. Na wakiomba msaadawatasaidiwa kwa kupewa maji kama mafuta yaliyo tibuka.Yatayo wababua nyuso zao. Kinywaji hicho ni kiovu mno!Na matandiko hayo ya kupumzikia ni maovu mno!
[18.30] Hakika wale walio amini na wakatenda mema - hakikaSisi hatupotezi ujira wa anaye tenda mema.
[18.31] Hao watapata Bustani za milele, zinazo pita mitokati yake. Humo watapambwa kwa mavazi ya mikononi yadhahabu, na watavaa nguo za kijani za hariri na at'ilasi, huku wakiegemea humo juu ya makochi. Nimalipo bora hayo! Na matandiko mazuri mno yakupumzikia!
[18.32] Na wapigie mfano wa watu wawili: mmoja wao tulimpavitalu viwili vya mizabibu, na tukavizungushiamitende, na kati yake tukatia mimea ya nafaka.
[18.33] Na hivyo vitalu viwili vikitoa mazao yake, walahapana kitu katika hayo kilicho tindikia. Na ndaniyake tukapasua mito.
[18.34] Naye alikuwa na mazao mengi. Basi akamwambiamwenzake naye akibishana naye: Mimi nimekushinda wewekwa mali na nguvu za watu!
[18.35] Na akaingia kitaluni kwake, naye hali anajidhulumunafsi yake. Akasema: Sidhani kabisa kuwa hayayataharibika.
[18.36] Wala sidhani kuwa hiyo Saa (ya Kyama) itatokea. Naikiwa nitarudishwa kwa Mola wangu Mlezi, bila ya shakanitapata marejeo bora zaidi kuliko haya.
[18.37] Mwenzake akamwambia kwa kubishana naye: Je!Unamkufuru aliye kuumba kutokana na udongo, tenakutokana na tone la manii, kisha akakufanya mtukaamili?
[18.38] Lakini Yeye Mwenyezi Mungu ndiye Mola wangu Mlezi.Wala simshirikishi na yeyote.
[18.39] Na lau kuwa ulipo ingia kitaluni kwako ungelisema: Mashaallah! Alitakalo Mwenyezi Mungu huwa!Hapana nguvu ila kwa Mwenyezi Mungu. Ikiwa unanionamimi nina mali kidogo na watoto kuliko wewe,
[18.40] Basi huenda Mola wangu Mlezi akanipa kilicho borakuliko kitalu chako, naye akapitisha kudra yake kutokambinguni kukilitea hicho chako, na kikageuka ardhi tupu inayo teleza.
[18.41] Au maji yake yakadidimia wala usiweze kuyagundua.
[18.42] Yakateketezwa matunda yake, akabaki akipinduapindua viganja vyake, kwa vile alivyo yagharimia, namiti imebwagika juu ya chanja zake. Akawa anasema:Laiti nisingeli mshiriki Mola wangu Mlezi na yeyote!
[18.43] Wala hakuwa nacho kikundi cha kumsaidia badala yaMwenyezi Mungu, wala mwenyewe hakuweza kujisaidia.
[18.44] Huko ulinzi ni wa Mwenyezi Mungu wa Haki tu. Yeyendiye mbora wa malipo, na mbora wa matokeo.
[18.45] Na wapigie mfano wa maisha ya dunia. Hayo ni kamamaji tunayo yateremsha kutoka mbinguni,yakachanganyika na mimea ya ardhi, kisha hiyo mimeaikawa vibuwa vinavyo peperushwa na upepo. Na MwenyeziMungu ni Mwenye uweza juu ya kila kitu.
[18.46] Mali na wana ni pambo la maisha ya dunia. Na memayanayo bakia ni bora mbele ya Mola wako Mlezi kwamalipo, na bora kwa matumaini.
[18.47] Na siku tutapo iondoa milima na ukaiona ardhiiwazi, na tukawafufua - wala hatutamwacha hata mmojakati yao -
[18.48] Na wakahudhurishwa mbele ya Mola wako Mlezi kwasafu (wakaambiwa): Mmetujia kama tulivyo kuumbeni maraya kwanza! Bali mlidai kwamba hatutakuwekeeni miadi.
[18.49] Na kitawekwa kitabu. Basi utawaona wakosefuwanavyo ogopa kwa yale yaliomo humo. Na watasema: Olewetu! Kitabu hichi kina nini! Hakiachi dogo wala kubwaila huliandika? Na watayakuta yote waliyo yatendayamehudhuria hapo. Na Mola wako Mlezi hamdhulumuyeyote.
[18.50] Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam!Walimsjudia isipo kuwa Iblisi. Yeye alikuwa miongonimwa majini, na akavunja amri ya Mola wake Mlezi. Je! Mnamshika yeye na dhuriya zake kuwa marafiki badalayangu, hali wao ni adui zenu? Ni ovu mno badala hiikwa wenye kudhulumu.
[18.51] Sikuwashuhudisha kuumbwa kwa mbingu na ardhi, walakuumbwa kwa nafsi zao. Wala sikuwafanya wapotezao kuwani wasaidizi.
[18.52] Na siku atakapo sema (Mwenyezi Mungu): Waiteni haomlio dai kuwa ni washirika wangu. Basi watawaita, nawao hawato waitikia. Nasi tutaweka baina yao maangamio.
[18.53] Na wakhalifu watauona Moto na watajua ya kwambawao lazima wataingia humo; wala hawatapata pakuuepuka.
[18.54] Na bila ya shaka tumewaelezea watu katika hiiQur'ani kila namna ya mfano. Lakini mwanaadamu amezidikuliko kila kitu kwa ubishi.
[18.55] Na hapana kilicho wazuia watu kuamini ulipo wajiauwongofu na wakaomba maghfira kwa Mola wao Mlezi,isipo kuwa yawafikie ya wale wa zamani, au iwafikie adhabu jahara.
[18.56] Na hatuwatumi Mitume ila wawe wabashiri nawaonyaji. Na walio kufuru wanabishana kwa uwongo, ilikwa uwongo huo waivunje kweli. Na wanazifanya Ishara zangu na yale waliyo onywa kuwa ni mzaha.
[18.57] Na ni nani dhaalimu mkubwa zaidi kuliko yule anayekumbushwa Ishara za Mola wake Mlezi, naye akazipuuzana akasahau yaliyo tangulizwa na mikono yake? Hakika Sisi tumeweka vifuniko juu ya nyoyo zao iliwasifahamu, na uziwi kwenye masikio yao. Na ukiwaitakwenye uwongofu hawakubali kabisa kuongoka.
[18.58] Na Mola wako Mlezi ni Msamehevu Mwenye rehema. Lauangeli wachukulia kwa mujibu waliyo yachuma, bila yashaka angeli wafanyia haraka kuwaadhibu. Lakini wanayo miadi ambayo hawatapata makimbilio yoyote yakuepukana nayo.
[18.59] Na miji hiyo tuliwaangamiza watu wake walipodhulumu. Na tukawawekea miadi ya maangamizo yao.
[18.60] Na pale Musa alipo mwambia kijana wake: Sitoachakuendelea mpaka nifike zinapo kutana bahari mbili, aunitaendelea kwa muda mrefu.
[18.61] Basi wawili hao walipo fika zinapo kutana hizobahari mbili walimsahau samaki wao, naye akashika njiayake kaporonyokea baharini.
[18.62] Walipo kwisha pita alimwambia kijana wake: Tupechakula chetu cha mchana. Kwa hakika tumepata machofukweli kwa hii safari yetu.
[18.63] Akasema (kijana): Waona! Pale tulipo pumzika penyejabali basi mimi nilimsahau yule samaki. Na hapanaaliye nisahaulisha nisimkumbuke ila Shet'ani tu. Naye akashika njia yake baharini kwa ajabu.
[18.64] (Musa) akasema: Hayo ndiyo tuliyo kuwa tunayataka.Basi wakarudi nyuma kwa kufuata njia waliyo jia.
[18.65] Basi wakamkuta mja katika waja wangu tuliye mparehema kutoka kwetu, na tukamfunza mafunzo yaliyo tokakwetu.
[18.66] Musa akamwambia: Nikufuate ili unifunze katika uleuwongofu ulio funzwa wewe?
[18.67] Akasema: Hakika wewe hutaweza kuvumilia kuwapamoja nami.
[18.68] Na utawezaje kuvumilia yale usiyo yajua vilivyoundani wake?
[18.69] Akasema: Inshaallah, Mwenyezi Mungu akipenda,utaniona mvumilivu, wala sitoasi amri yako.
[18.70] Akasema: Basi ukinifuata usiniulize kitu mpakamimi nianze kukutajia.
[18.71] Basi wawili hao wakatoka, hata walipo panda jahazi(yule mtu) akaitoboa. (Musa) akasema: Unaitoboauwazamishe watu wake? Hakika umefanya jambo baya.
[18.72] Akasema: Sikukwambia hutaweza kuvumilia kuwapamoja nami?
[18.73] (Musa) akasema: Usinichukulie kwa niliyo sahau,wala usinipe uzito kwa jambo langu.
[18.74] Basi wakatoka wawili hao mpaka wakamkuta kijana,akamuuwa. (Musa) akasema: Ala! Umemuuwa mtu asiye nakosa, na wala hakuuwa! Ama hakika umefanya jambo baya kabisa!
[18.75] AKASEMA: Je! Sikukwambia kwamba hakika wewe huwezikuvumilia kuwa pamoja nami?
[18.76] Akasema: Nikikuuliza kitu chochote baada ya hayausifuatane nami, kwani umekwisha pata udhuru kwangu.
[18.77] Basi wakatoka mpaka wakawafikia watu wa mji mmoja.Wakawaomba watu wake wawape chakula, nao wakakataakuwakaribisha. Hapo wakakuta ukuta unataka kuanguka, (yule mja mwema) akausimamisha. (Musa)akasema: Ungeli taka ungeli chukua ujira kwa haya.
[18.78] (Yule mtu) akasema: Huku ndio kufarikiana bainayangu na wewe. Sasa nitakueleza maana ya yale uliyokuwa huwezi kuyastahamilia.
[18.79] Ama ile jahazi ilikuwa ya masikini za Munguwafanyao kazi baharini. Nilitaka kuiharibu, kwaninyuma yao alikuwako mfalme anaghusubu majahazi yote.
[18.80] Na ama yule kijana, wazazi wake walikuwa niWaumini. Tukakhofu asije watia mashakani kwa uasi naukafiri.
[18.81] Basi tulitaka Mola wao Mlezi awabadilishie aliyebora zaidi kuliko huyo kwa kutakasika, na aliye karibuzaidi kwa huruma.
[18.82] Na ama ukuta, huo ulikuwa ni wa vijana wawilimayatima kule mjini. Na chini yake ilikuwako khazinayao; na baba yao alikuwa ni mtu mwema. Basi Mola wako Mlezi alitaka wafikie utu uzima na wajitolee khazinayao wenyewe, kuwa ni rehema itokayo kwa Mola wakoMlezi. Wala mimi sikutenda hayo kwa amri yangu. Hiyondiyo tafsiri ya hayo ambayo wewe hukuwezakuyasubiria.
[18.83] Na wanakuuliza khabari za Dhul- Qarnaini. Waambie:Nitakusimulieni baadhi ya hadithi yake.
[18.84] Sisi tulimtilia nguvu katika ardhi na tukampa njiaza kila kitu.
[18.85] Basi akaifuata njia.
[18.86] Hata alipo fika machwea-jua aliliona linatuakatika checmchem yenye matope meusi. Na hapo akawakutawatu. Tukasema: Ewe Dhul-Qarnaini! Ama uwaadhibu au watwae kwa wema.
[18.87] Akasema: Ama aliye dhulumu basi tutamuadhibu, nakisha atarudishwa kwa Mola wake Mlezi amuadhibu adhabuisiyo juulikana.
[18.88] Na ama aliye amini na akatenda mema basi atapatamalipo mazuri. Nasi tutamwambia lilio jepesi katikaamri yetu.
[18.89] Kisha akaifuata njia.
[18.90] Hata alipo fika matokeo ya jua alilionalinawachomozea watu tusio wawekea pazia la kuwakinganalo.
[18.91] Ndio hivyo hivyo. Na Sisi tulizijua vilivyokhabari zake zote.
[18.92] Kisha akaifuata njia.
[18.93] Hata alipo fika baina ya milima miwili, alikutanyuma yake watu ambao takriban hawakuwa wanafahamulolote.
[18.94] Wakasema: Ewe Dhul-Qarnaini! HakikaJuju-wa-maajuju wanafanya uharibifu katika nchi. Basije, tukulipe ujira ili utujengee baina yetu na waongome?
[18.95] Akasema: Yale Mola wangu aliyo niwezesha ni borazaidi. Lakini nyinyi nisaidieni kwa nguvu zenu.Nitakujengeeni kizuizi baina yenu na wao.
[18.96] Nileteeni vipande vya chuma. Hata alipo ijazanafasi iliyo kati ya milima miwili, akasema: Vukuteni.Hata alipo kifanya (chuma) kama moto akasema: Nileteeni shaba iliyo yayuka niimwagie.
[18.97] Basi hawakuweza kuukwea, wala hawakuweza kuutoboa.
[18.98] Akasema: Hii ni rehema itokayo kwa Mola wanguMlezi. Na itapo fika ahadi ya Mola wangu Mleziatauvunja vunja. Na ahadi ya Mola wangu Mlezi ni kwelitu.
[18.99] Na siku hiyo tutawaacha wakisongana wao kwa wao.Na baragumu litapulizwa, na wote watakusanywa pamoja.
[18.100] Na siku hiyo tutawadhihirishia wazi Jahannamumakafiri waione.
[18.101] Wale ambao kwamba macho yao yalikuwa pazianihayanikumbuki, na wakawa hawawezi kusikia.
[18.102] Je, wanadhani walio kufuru ndio wawafanye wajawangu ndio walinzi wao badala yangu Mimi? Hakika Sisitumeiandaa Jahannamu iwe ndipo mahala pa kuteremkia makafiri.
[18.103] Sema: Je, tukutajieni wenye khasara mno katikavitendo vyao?
[18.104] Ni wale ambao juhudi yao katika maisha ya duniaimepotea bure, nao wanadhani kwamba wanafanya kazinzuri.
[18.105] Hao ni wale walio zikanusha Ishara za Mola waoMlezi na kukutana naye. Kwa hivyo vitendo vyaovimepotea bure, na wala Siku ya Kiyama hatutawathaminikitu.
[18.106] Hiyo Jahannamu ni malipo yao kwa walivyo kufuruna wakafanyia kejeli Ishara zangu na Mitume wangu.
[18.107] Hakika wale walio amini na wakatenda memamashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi.
[18.108] Watadumu humo; hawatataka kuondoka.
[18.109] Sema: Lau kuwa bahari ndio wino kwa maneno yaMola wangu Mlezi, basi bahari ingeli malizika kabla yakumalizika maneno ya Mola wangu Mlezi, hata tungeli ileta mfano wa hiyo kuongezea.
[18.110] Sema: Mimi ni mwanaadamu kama nyinyi. NinaletewaWahyi kwamba Mungu wenu ni Mungu Mmoja. Mwenyekutaraji kukutana na Mola wake Mlezi basi naatendevitendo vyema, wala asimshirikishe yeyote katika ibadaya Mola wake Mlezi.
Featured Ad
About Us
Contact Us
Advertise
Donate
Bookmark Us
Support Us
GuestBook
Link To Us
Newsletter
Recommend
Set as Home
Terms Of Use
What's New
Other Sites:
Know The Prophet campaign
-
Discover Islam
-
Pharmacy Site
-
Links SQL Plugins
This Page Was Last Updated on
Copyright 2003-2008
Islamic Education & Services Institute