Skip to Content
The Muslims Internet Directory
Featured Service
Home
|
Advertise
|
FAQ
|
Login/Register |
Directory
Quran
Hadith
Islamic Library
Prayer Times
Discover Islam
Islamic Gallery
Calendar
New
Classifieds
Services
Webmasters
Dictionary
Downloads
Kids & Games
Quran Navigation
Search
Translations
Transliteration
Index
Chapter Info
English Search
Articles and Books
Audio
Memorization
Links
Downloads
On Your Site
FAQ
Muslims Internet Directory
The Quran / English
The Hadith
2Muslims.com
Our Network
Islamic Library & Articles
The Internet
Islamic Classifieds
WebRing Members Sites
Advance
-
Live Search
-
Quran
-
Hadith
-
Search This Site
-
The Network
-
Classifieds
-
WebRing
-
The Internet
-
Help!
Featured Site
Feature Your Site Now
2Muslims Services
Islamic IE Toolbar
Islamic Internet Gadgets
Prayer Times Software
Forum
Donate
Islamic Quizzes
Islamic CGI Scripts
Polls
Free E-mail Account
Zakat Calculator
Islamic Holidays Dates
Islamic Date Converter
DAWA Tools
FAQ About Islam
Buy The Islamic CD
God's Attributes
How To Pray?
Paid Services
Buy The Islamic CD
Banner Design
Submit Your Site
Muslims Million Pixels
Translate Site To:
Arabic
Bulgarian
Catalan
Chinese (Simplified)
Chinese (Traditional)
Croatian
Czech
Danish
Dutch
English
Filipino
Finnish
French
German
Greek
Hebrew
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latvian
Lithuanian
Norwegian
Polish
Portuguese
Romanian
Russian
Serbian
Slovak
Slovenian
Spanish
Swedish
Ukrainian
Vietnamese
Hijab
Why do muslim females wear Hijab (Head cover)?
Faith
Culture
Fear
Other
view results
view other polls
Home
:
Quran:
Quran Translations:
Swahili:
SURATUN NUR :
Search the Quran in any of the drop down menu languages:
--Select language--
Albanian
Arabic
Azerbaijani
Bengali
Bosnian
Brazilian
Burmese
Chinese
Dutch
English_Abdullah_Yusuufali
English_Hasan_Qaribullah
English_Muhammad_Pickthall
Farsi
Finish
French
German
Hausa
Hindi
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latin
Malaysian
Melayu
Meranao
Mexican
Pashto
Persian
Poland
Portuguese
Russian
Spanish
Swahili
Tamil
Thai
Transliteration
Turkish
Urdu
More search options
SURATUN NUR
[24.1] HII NI SURA Tuliyo iteremsha na tukailazimisha;tukateremsha ndani yake Aya zilizo wazi ili mkumbuke.
[24.2] Mzinifu mwanamke na mzinifu mwanamume, mtandikenikila mmoja katika wao bakora mia. Wala isikushikenihuruma kwa ajili yao katika hukumu ya Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi mnamuamini Mwenyezi Mungu na Sikuya Mwisho. Na lishuhudie adhabu yao kundi la Waumini.
[24.3] Mwanamume mzinifu hamwoi ila mwanamke mzinifu aumwanamke mshirikina. Na mwanamke mzinifu haolewi ilana mwanamume mzinifu au mshirikina. Na hayo yameharimishwa kwa Waumini.
[24.4] Na wanao wasingizia wanawake mahashumu, kishawasilete mashahidi wane, basi watandikeni bakorathamanini, na msiwakubalie ushahidi wao tena. Na haondio wapotovu.
[24.5] Isipo kuwa wale walio tubu baada ya hayo nawakatengenea; kwani bila ya shaka Mwenyezi Mungu niMsamehevu, Mwenye kurehemu.
[24.6] Na wale wanao wasingizia wake zao na hawanamashahidi ila nafsi zao, basi ushahidi wa mmoja waoutakuwa kushuhudilia mara nne kwa kiapo cha MwenyeziMungu ya kwamba hakika yeye ni katika wasema kweli.
[24.7] Na mara ya tano kwamba laana ya Mwenyezi Mungu iwejuu yake ikiwa ni miongoni mwa waongo.
[24.8] Na mke itamwondokea adhabu kwa kutoa shahada maranne kwa kiapo cha Mwenyezi Mungu ya kwamba huyu mumeni miongoni mwa waongo.
[24.9] Na mara ya tano ya kwamba ghadhabu ya MwenyeziMungu iwe juu yake kama mumewe yu miongoni mwa wanaosema kweli.
[24.10] Na lau kuwa si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yenuna rehema yake, na ya kuwa Mwenyezi Mungu ni Mpokeajitoba....
[24.11] Hakika wale walio leta uwongo ni kundi miongonimwenu. Msifikiri ni shari kwenu, bali hiyo ni kherikwenu. Kila mtu katika wao atapata aliyo yachuma katika madhambi. Na yule aliyejitwika sehemu yakekubwa miongoni mwao, atapata adhabu kubwa.
[24.12] Kwa nini mlipo sikia khabari hii, wanaume Wauminina wanawake Waumini hawakuwadhania wenzao mema, nakusema: Huu ni uzushi dhaahiri?
[24.13] Kwa nini hawakuleta mashahidi wane? Na ilivyo kuwahawakuleta mashahidi wane basi hao mbele ya MwenyeziMungu ni waongo.
[24.14] Na lau kuwa si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yenuna rehema yake katika dunia na Akhera, bila ya shakaingeli kupateni adhabu kubwa kwa sababu ya yale mliyo jiingiza.
[24.15] Mlipo yapokea kwa ndimi zenu na mkasema kwa vinywavyenu msiyo yajua, na mlifikiri ni jambo dogo, kumbembele ya Mwenyezi Mungu ni kubwa.
[24.16] Na kwa nini mlipo yasikia msiseme: Haitufaliikuzungumza haya. Subhanak Umetakasika! Huu ni uzushimkubwa!
[24.17] Mwenyezi Mungu anakuonyeni msirejee tena kufanyakama haya kabisa, ikiwa nyinyi ni Waumini!
[24.18] Na Mwenyezi Mungu anakubainisheni Aya. Na MwenyeziMungu ni Mjuzi Mwenye hikima.
[24.19] Kwa hakika wale wanao penda uenee uchafu kwa walioamini, watapata adhabu chungu katika dunia na Akhera.Na Mwenyezi Mungu anajua na nyinyi hamjui.
[24.20] Na lau kuwa si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yenuna rehema yake, na kuwa hakika Mwenyezi Mungu niMpole, Mwenye kurehemu....
[24.21] Enyi mlio amini! Msizifuate nyayo za Shet'ani. Naatakaye fuata nyayo za Shet'ani basi yeye huamrishamachafu na maovu. Na lau kuwa si fadhila ya Mwenyezi Mungu na rehema yake juu yenu, asingelitakasika miongoni mwenu kabisa hata mmoja. LakiniMwenyezi Mungu humtakasa amtakaye, na Mwenyezi Munguni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.
[24.22] Na wale katika nyinyi wenye fadhila na wasaawasiape kutowapa jamaa zao na masikini na walio hamakwa Njia ya Mwenyezi Mungu. Na wasamehe, na waachilie mbali. Je! Nyinyi hampendi Mwenyezi Mungu akusameheni?Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
[24.23] Hakika wanao wasingizia wanawake, wanao jihishimu,walio ghafilika, Waumini, wamelaaniwa duniani naAkhera, nao watapata adhabu kubwa.
[24.24] Siku ambayo zitawashuhudia ndimi zao na mikono yaona miguu yao kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
[24.25] Siku hiyo Mwenyezi Mungu atawapa sawa sawa malipoyao ya haki, na watajua kwamba hakika Mwenyezi Mungundiye Haki Iliyo Wazi.
[24.26] Wanawake waovu ni wa wanaume waovu, na wanaumewaovu ni wa wanawake waovu. Na wanawake wema ni wawanaume wema, na wanaume wema ni wa wanawake wema. Haowameepushwa na hayo wanayo yasema; wao watapatamsamaha na riziki ya ukarimu.
[24.27] Enyi mlio amini! Msiingie nyumba zisio nyumba zenumpaka mwombe ruhusa, na mwatolee salamu wenyewe. Hayoni bora kwenu mpate kukumbuka.
[24.28] Na msipo mkuta mtu humo basi msiingie mpakamruhusiwe. Na mkiambiwa: Rudini! Basi rudini. Hivi niusafi zaidi kwenu. Na Mwenyezi Mungu anajua mnayoyatenda.
[24.29] Si vibaya kwenu kuingia nyumba zisio kaliwa ambazondani yake yamo manufaa yenu. Na Mwenyezi Mungu anajuamnayo yadhihirisha na mnayo yaficha.
[24.30] Waambie Waumini wanaume wainamishe macho yao, nawazilinde tupu zao. Hili ni takaso bora kwao. HakikaMwenyezi Mungu anazo khabari za wanayo yafanya.
[24.31] Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao,na wazilinde tupu zao, wala wasionyeshe uzuri waoisipo kuwa unao dhihirika. Na waangushe shungi zao juu ya vifua vyao, wala wasionyeshe uzuri wao ila kwawaume zao, au baba zao, au baba wa waume zao, auwatoto wao, au watoto wa waume zao, au kaka zao, auwana wa kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawakewenzao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, auwafwasi wanaume wasio na matamanio, au watoto ambaohawajajua mambo yaliyo khusu uke. Wala wasipige chinimiguu yao ili yajuulikane mapambo waliyo yaficha. Natubuni nyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ilimpate kufanikiwa.
[24.32] Na waozeni wajane miongoni mwenu na wema katikawatumwa wenu na wajakazi wenu. Wakiwa mafakiriMwenyezi Mungu atawatajirisha kwa fadhila yake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa Mwenye kujua.
[24.33] Na wajizuilie na machafu wale wasio pata chakuolea, mpaka Mwenyezi Mungu awatajirishe kwa fadhilayake. Na wanao taka kuandikiwa uhuru katika wale ambaomikono yenu ya kulia imewamiliki, basi waandikienikama mkiona wema kwao. Na wapeni katika mali yaMwenyezi Mungu aliyo kupeni. Wala msiwashurutishevijakazi vyenu kufanya zina kwa ajili ya kutafuta patola maisha ya dunia, ilhali wao wanataka kujihishimu.Na atakaye walazimisha basi Mwenyezi Mungu baada ya kulazimishwa kwao huko, atawasamehe, kwani MwenyeziMungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
[24.34] Na kwa yakini tumekuteremshieni Ishara zilizo wazina mifano kutokana na walio tangulia kabla yenu namawaidha kwa wachamngu.
[24.35] Mwenyezi Mungu ni Nuru ya Mbingu na Ardhi. Mfanowa Nuru yake ni kama shubaka lenye kuwekwa ndani yaketaa. Taa ile imo katika tungi. Tungi lile ni kama nyota inayo meremeta, inayo washwa kwa mafutayanayo toka katika mti ulio barikiwa, mzaituni. Si wamashariki wala magharibi. Yanakaribia mafuta yake kung'aa wenyewe ingawa moto haujayagusa - Nuru juu yaNuru. Mwenyezi Mungu humwongoa kwenye Nuru yakeamtakaye. Na Mwenyezi Mungu huwapigia watu mifano. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua kila kitu.
[24.36] Katika Nyumba ambazo Mwenyezi Mungu ameamrishazitukuzwe, na humo litajwe jina lake, wanamtakasa humoasubuhi na jioni
[24.37] Watu ambao biashara wala kuuza hakuwashughulishina kumdhukuru Mwenyezi Mungu, na kushika Sala, nakutoa Zaka. Wanaikhofu Siku ambayo nyoyo na macho yatageuka.
[24.38] Ili Mwenyezi Mungu awalipe bora ya waliyo yatenda,na awazidishie katika fadhila zake. Na Mwenyezi Munguhumruzuku amtakaye bila ya hisabu.
[24.39] Na walio kufuru vitendo vyao ni kama sarabi(mazigazi) uwandani. Mwenye kiu huyadhania ni maji.Hata akiyaendea hapati chochote. Na atamkuta MwenyeziMungu hapo naye amlipe hisabu yake sawa sawa. NaMwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.
[24.40] Au ni kama giza katika bahari kuu, iliyo funikwana mawimbi juu ya mawimbi, na juu yake yapo mawingu.Giza juu ya giza. Akiutoa mtu mkono wake anakaribia asiuone. Na ambaye Mwenyezi Mungu hakumjaalia kuwa nanuru hawi na nuru.
[24.41] Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu vinamtakasavilivyomo katika mbingu na ardhi, na ndege wakikunjuambawa zao? Kila mmoja amekwisha jua Sala yake na namna ya kumtakasa kwake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenyekuyajua wayatendayo.
[24.42] Na ni wa Mwenyezi Mungu ufalme wa mbingu na ardhi,na kwa Mwenyezi Mungu ndio marejeo ya wote.
[24.43] Je! Huoni ya kwamba Mwenyezi Mungu huyasukumamawingu, kisha huyaambatisha, kisha huyafanya mirundi?Basi utaona mvua ikitoka kati yake. Na huteremsha kutoka juu kwenye milima ya mawingu mvua ya mawe,akamsibu nayo amtakaye na akamuepusha nayo amtakaye.Hukurubia mmetuko wa umeme wake kupofua macho.
[24.44] Mwenyezi Mungu hubadilisha usiku na mchana. Hakikakatika hayo yapo mazingatio kwa wenye kuona.
[24.45] Na Mwenyezi Mungu ameumba kila kinyama kutokana namaji. Wengine katika wao huenda kwa matumbo yao, nawengine huenda kwa miguu miwili, na wengine huenda kwa miguu mine. Mwenyezi Mungu huumba ayatakayo.Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.
[24.46] Kwa yakini tumeteremsha Ishara zinazo bainisha. NaMwenyezi Mungu hummwongoa amtakaye kwenye Njia IliyoNyooka.
[24.47] Na wanasema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na Mtume,na tumet'ii. Kisha kikundi katika hao hugeuka baada yahayo. Wala hao si wenye kuamini.
[24.48] Na wanapo itwa kumuendea Mwenyezi Mungu na Mtumewake ili ahukumu baina yao, kipo kikundi katika waokinakataa.
[24.49] Na ikiwa haki ni yao, wanamjia kwa kut'ii.
[24.50] Je! Wana maradhi katika nyoyo zao, au wanaonashaka, au wanaogopa ya kuwa Mwenyezi Mungu na Mtumewake watawadhulumu? Bali hao ndio madhaalimu.
[24.51] Haiwi kauli ya Waumini wanapo itwa kwa MwenyeziMungu na Mtume wake ili ahukumu baina yao, ila nikusema: Tumesikia, na tumet'ii! Na hao ndio wenye kufanikiwa.
[24.52] Na wenye kumt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, nawakamwogopa Mwenyezi Mungu na wakamcha, basi hao ndiowenye kufuzu.
[24.53] Na wanaapa kwa Mwenyezi Mungu ukomo wa kiapo chaoya kwamba ukiwaamrisha kwa yakini watatoka. Sema:Msiape! Ut'iifu unajuulikana. Hakika Mwenyezi Munguanazo khabari za mnayo yatenda.
[24.54] Sema: Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume. Namkigeuka, basi yaliyo juu yake ni aliyo bebeshwa, nayaliyo juu yenu ni mliyo bebshwa nyinyi. Na mkimt'ii yeye mtaongoka. Na hapana juu ya Mtume ila kufikishaUjumbe wazi wazi.
[24.55] Mwenyezi Mungu amewaahidi wale walio aminimiongoni mwenu na wakatenda mema, ya kwamba atawafanyamakhalifa katika ardhi kama alivyo wafanya makhalifawa kabla yao, na kwa yakini atawasimamishia Dini yaoaliyo wapendelea, na atawabadilishia amani baada yakhofu yao. Wawe wananiabudu Mimi, wala wasinishirikishe na chochote. Na watao kufuru baada yahayo, basi hao ndio wapotovu.
[24.56] Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na mt'iini Mtume,ili mpate kurehemewa.
[24.57] Msiwadhanie walio kufuru kwamba watashinda katikanchi. Na makaazi yao ni Motoni, na hakika ni maovukweli marejeo yao.
[24.58] Enyi mlio amini! Nawakutakeni idhini iliyowamiliki mikono yenu ya kulia na walio bado kubaalighimiongoni mwenu mara tatu - kabla ya Sala ya alfajiri,na wakati mnapo vua nguo zenu adhuhuri, na baada yaSala ya isha. Hizi ni nyakati tatu za faragha kwenu.Si vibaya kwenu wala kwao baada ya nyakati hizi, kuzungukiana nyinyi kwa nyinyi. Hivyo ndivyo MwenyeziMungu anavyo kuelezeni Aya zake, na Mwenyezi Mungu niMjuzi Mwenye hikima.
[24.59] Na watoto wanapo fikilia umri wa kubaalighi basinawatake ruhusa, kama walivyo taka ruhusa wa kablayao. Hivyo ndivyo anavyo kubainishieni Mwenyezi Mungu Aya zake, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenyehikima.
[24.60] Na wanawake wazee wasio taraji kuolewa, si vibayakwao kupunguza nguo zao, bila ya kujishaua kwamapambo. Na wakijihishimu ni bora kwao. Na MwenyeziMungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.
[24.61] Si vibaya kwa kipofu, wala si vibaya kwa kiguru,wala si vibaya kwa mgonjwa, wala kwenu nyinyi, mkilakatika nyumba zenu, au nyumba za baba zenu, au nyumba za mama zenu, au nyumba za kaka zenu, au nyumba zadada zenu, au nyumba za ami zenu, au nyumba zashangazi zenu, au nyumba za wajomba zenu, au nyumba zadada wa mama zenu, au za mlio washikia funguo zao, aurafiki yenu. Si vibaya kwenu mkila pamoja au mbalimbali. Na mkiingia katika nyumba, toleaneni salamu,kuwa ni maamkio yanayo toka kwa Mwenyezi Mungu, yenyebaraka na mema. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyokubainishieni Aya zake mpate kuelewa.
[24.62] Hakika Waumini wa kweli ni walio muamini MwenyeziMungu na Mtume wake; na wanapo kuwa pamoja naye kwajambo la kuwakhusu wote hawaondoki mpaka wamtake ruhusa. Kwa hakika wale wanao kuomba ruhusa, hao ndiowanao muamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Nawakikuomba ruhusa kwa baadhi ya kazi zao, mruhusu umtakaye miongoni mwao, uwaombee msamaha kwa MwenyeziMungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe,Mwenye kurehemmu.
[24.63] Msifanye wito wa Mtume baina yenu kama wito wanyinyi kwa nyinyi. Hakika Mwenyezi Mungu anawajuamiongoni mwenu wanao ondoka kwa uficho. Basi nawatahadhari wanao khalifu amri yake, usije ukawapatamsiba au ikawapata adhabu chungu.
[24.64] Jueni kuwa hakika ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomombinguni na ardhini. Hakika Yeye anajua mlio nayo. Nasiku mtapo rudishwa kwake atawaeleza waliyo yafanya. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
Featured Ad
About Us
Contact Us
Advertise
Donate
Bookmark Us
Support Us
GuestBook
Link To Us
Newsletter
Recommend
Set as Home
Terms Of Use
What's New
Other Sites:
Know The Prophet campaign
-
Discover Islam
-
Pharmacy Site
-
Links SQL Plugins
This Page Was Last Updated on
Copyright 2003-2008
Islamic Education & Services Institute