Skip to Content
The Muslims Internet Directory
Featured Service
Home
|
Advertise
|
FAQ
|
Login/Register |
Directory
Quran
Hadith
Islamic Library
Prayer Times
Discover Islam
Islamic Gallery
Calendar
New
Classifieds
Services
Webmasters
Dictionary
Downloads
Kids & Games
Quran Navigation
Search
Translations
Transliteration
Index
Chapter Info
English Search
Articles and Books
Audio
Memorization
Links
Downloads
On Your Site
FAQ
Muslims Internet Directory
The Quran / English
The Hadith
2Muslims.com
Our Network
Islamic Library & Articles
The Internet
Islamic Classifieds
WebRing Members Sites
Advance
-
Live Search
-
Quran
-
Hadith
-
Search This Site
-
The Network
-
Classifieds
-
WebRing
-
The Internet
-
Help!
Featured Site
Feature Your Site Now
2Muslims Services
Islamic IE Toolbar
Islamic Internet Gadgets
Prayer Times Software
Forum
Donate
Islamic Quizzes
Islamic CGI Scripts
Polls
Free E-mail Account
Zakat Calculator
Islamic Holidays Dates
Islamic Date Converter
DAWA Tools
FAQ About Islam
Buy The Islamic CD
God's Attributes
How To Pray?
Paid Services
Buy The Islamic CD
Banner Design
Submit Your Site
Muslims Million Pixels
Translate Site To:
Arabic
Bulgarian
Catalan
Chinese (Simplified)
Chinese (Traditional)
Croatian
Czech
Danish
Dutch
English
Filipino
Finnish
French
German
Greek
Hebrew
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latvian
Lithuanian
Norwegian
Polish
Portuguese
Romanian
Russian
Serbian
Slovak
Slovenian
Spanish
Swedish
Ukrainian
Vietnamese
Hijab
Why do muslim females wear Hijab (Head cover)?
Faith
Culture
Fear
Other
view results
view other polls
Home
:
Quran:
Quran Translations:
Swahili:
SURAT AL A'NKABUT :
Search the Quran in any of the drop down menu languages:
--Select language--
Albanian
Arabic
Azerbaijani
Bengali
Bosnian
Brazilian
Burmese
Chinese
Dutch
English_Abdullah_Yusuufali
English_Hasan_Qaribullah
English_Muhammad_Pickthall
Farsi
Finish
French
German
Hausa
Hindi
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latin
Malaysian
Melayu
Meranao
Mexican
Pashto
Persian
Poland
Portuguese
Russian
Spanish
Swahili
Tamil
Thai
Transliteration
Turkish
Urdu
More search options
SURAT AL A'NKABUT
[29.1] Alif Lam Mim (A.L.M.)
[29.2] Je! Wanadhani watu wataachwa kwa kuwa wanasema:Tumeamini. Nao wasijaribiwe?
[29.3] Hakika tuliwajaribu walio kuwa kabla yao, na kwayakini Mwenyezi Mungu atawatambulisha walio wa kwelina atawatambulisha walio waongo.
[29.4] Au wanadhani wanao tenda maovu kwamba watatushinda?Hukumu mbaya hiyo wanayo hukumu.
[29.5] Mwenye kutaraji kukutana na Mwenyezi Mungu, basihakika miadi ya Mwenyezi Mungu itafika bila ya shaka.Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.
[29.6] Na anaye fanya juhudi basi bila ya shaka anafanyajuhudi kwa ajili ya nafsi yake. Hakika Mwenyezi Mungusi mhitaji wa walimwengu.
[29.7] Na walio amini na wakatenda mema, kwa yakinitutawafutia makosa yao, na tutawalipa bora ya waliyokuwa wakiyatenda.
[29.8] Na tumemuusia mwanaadamu kuwafanyia wema wazaziwake. Na ikiwa watakushikilia unishirikishe Mimi nausiyo kuwa na ujuzi nayo, basi usiwat'ii. Kwangu Mimindio marejeo yenu, na nitakwambieni mliyo kuwamkiyatenda.
[29.9] Na walio amini na wakatenda mema, bila ya shakatutawatia miongoni mwa watu wema.
[29.10] Na katika watu wapo wanao sema: TumemuaminiMwenyezi Mungu. Lakini wanapo pewa maudhi kwa ajili yaMwenyezi Mungu, wanayafanya mateso ya watu kama ni adhabu ya Mwenyezi Mungu. Na inapo kuja nusura kutokakwa Mola wako Mlezi husema: Hakika sisi tulikuwapamoja nanyi. Kwani Mwenyezi Mungu hayajui yaliomo vifuani mwa walimwengu?
[29.11] Na hapana shaka Mwenyezi Mungu atawatambulishawalio amini, na atawatambulisha wanaafiki.
[29.12] Na walio kufuru waliwaambia walio amini: Fuateninjia yetu, nasi tutayabeba makosa yenu. Wala waohawatabeba katika makosa yao chochote kile. Hakika haoni waongo.
[29.13] Na hapana shaka wataibeba mizigo yao na mizigomingine pamoja na mizigo yao. Na kwa yakini wataulizwaSiku ya Kiyama juu ya waliyo kuwa wakiyazua.
[29.14] Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, na akakaanao miaka elfu kasoro miaka khamsini. Basi tufanililiwachukua, nao ni madhaalimu.
[29.15] Nasi tukamwokoa yeye na wenziwe wa katika safina,na tukaifanya kuwa ni Ishara kwa walimwengu wote.
[29.16] Na Ibrahim pale alipo waambia watu wake: MuabuduniMwenyezi Mungu, na mcheni Yeye. Hiyo ndiyo kheri yenu,ikiwa nyinyi mnajua.
[29.17] Hakika nyinyi mnaabudu masanamu badala ya MwenyeziMungu, na mnazua uzushi. Hakika hao mnao waabudubadala ya Mwenyezi Mungu hawakumilikiini rizikiyoyote. Takeni riziki kwa Mwenyezi Mungu, na mumuabuduYeye, na mumshukuru Yeye. Kwake Yeye ndio mtarudishwa.
[29.18] Na mkikadhibisha, basi kaumu kadhaa wa kadhaa zakabla yenu zilikwisha kadhibisha. Na si juu ya Mtumeila kufikisha Ujumbe waziwazi.
[29.19] Je! Wao hawaoni jinsi Mwenyezi Mungu anavyoanzisha uumbaji, na kisha akarudisha tena. Hakika hayokwa Mwenyezi Mungu ni mepesi.
[29.20] Sema: Tembeeni katika ardhi na tazameni jinsialivyo anzisha uumbaji; kisha Mwenyezi Mungu ndiyeanaye umba umbo la baadaye. Hakika Mwenyezi Mungu niMuweza juu ya kila kitu.
[29.21] Humuadhibu amtakaye, na humrehemu amtakaye. Nakwake Yeye mtapelekwa.
[29.22] Na nyinyi si wenye kushinda katika ardhi walakatika mbingu. Wala nyinyi hamna mlinzi wala msaidiziisipo kuwa Mwenyezi Mungu.
[29.23] Na walio zikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu nakukutana naye, hao ndio wenye kukata tamaa na rehemayangu, na hao ndio wenye kupata adhabu chungu.
[29.24] Basi haikuwa jawabu ya watu wake ila ni kusema:Muuweni au mchomeni moto! Mwenyezi Mungu akamwokoa namoto. Hakika katika hayo zipo Ishara kwa watu wanao amini.
[29.25] Na alisema: Hakika nyinyi mmeyashika masanamubadala ya Mwenyezi Mungu kwa mapenzi yaliyo baina yenukatika uhai wa duniani. Kisha Siku ya Kiyama mtakataana nyinyi kwa nyinyi, na mtalaaniana nyinyikwa nyinyi. Na makaazi yenu ni Motoni. Wala hamtapatawa kukunusuruni.
[29.26] Lut'i akamuamini, na akasema: Mimi nahamia kwaMola wangu Mlezi. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu,Mwenye hikima.
[29.27] Na tulimtunukia (Ibrahim) Is-haq na Yaa'qub. Natukajaalia katika dhuriya zake Unabii na Kitabu, natukampa ujira wake katika dunia; naye hakika katika Akhera bila ya shaka ni katika watu wema.
[29.28] Na pale Lut'i alipo waambia watu wake: Hakikanyinyi mnafanya uchafu, ambao hapana mmoja katikawalimwengu aliye kutangulieni kwa hayo.
[29.29] Je! Nyinyi mnawaingilia wanaume, na mnaikata njia?Na katika mikutano yenu mnafanya maovu? Basi haikuwajawabu ya watu wake isipo kuwa kusema: Tuletee hiyo adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwa wewe ni katika wasemaokweli.
[29.30] Akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Ninusuru na watumafisadi hawa!
[29.31] Na wajumbe wetu walipo mjia Ibrahim na bishara,walisema: Hakika sisi hapana shaka tutawahiliki watuwa mji huu, kwani watu wake hakika wamekuwamadhaalimu.
[29.32] Akasema: Hakika humo yumo Lut'i. Wao wakasema:Sisi tunajua zaidi nani yumo humo. Hapana shakatutamwokoa yeye na ahali zake, isipo kuwa mkewe aliye miongoni mwa watao kaa nyuma.
[29.33] Na wajumbe wetu walipo mfikia Lut'i, alihuzunikakwa ajili yao, na moyo uliona dhiki kwa ajili yao.Wakasema: Usiogope, wala usihuzunike. Hakika sisi tutakuokoa wewe na ahali zako, ila mkeo aliye miongonimwa watao kaa nyuma.
[29.34] Kwa yakini sisi tutawateremshia watu wa mji huuadhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya uchafu wanaoufanya.
[29.35] Na tumeacha katika mji huo Ishara ilio wazi kwawatu wanao tumia akili zao.
[29.36] Na kwa Madyana tulimtuma ndugu yao Shuaibu, nayeakasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu naiogopeni Siku ya Akhera, wala msende katika ardhi mkifisidi.
[29.37] Lakini walimkanusha basi ukawatwaa mtikiso waardhi, wakapambazukiwa ndani ya nyumba zao naowamefudikia.
[29.38] Na pia kina A'di na Thamud. Nanyi yamekwishakubainikieni kutokana na maskani zao. Na Shet'anialiwapambia vitendo vyao, na akawazuilia Njia, na haliwalikuwa wenye kuona.
[29.39] Na pia Qaruni na Firauni na Hamana! Na Musaaliwajia kwa Ishara waziwazi, lakini walijivuna katikanchi, wala hawakuweza kushinda.
[29.40] Basi kila mmoja tulimtesa kwa mujibu wa makosayake. Kati yao wapo tulio wapelekea kimbunga chachangarawe; na kati yao wapo walio nyakuliwa naukelele; na kati yao wapo ambao tulio wadidimizakatika ardhi; na kati yao wapo tulio wazamisha. WalaMwenyezi Mungu hakuwa mwenye kuwadhulumu, lakiniwalikuwa wenyewe wakijidhulumu nafsi zao.
[29.41] Mfano wa walio wafanya walinzi badala ya MwenyeziMungu, ni mfano wa buibui alivyo jitandia nyumba. Nahakika nyumba dhaifu mno kuliko zote ni jumba la buibui, laiti kuwa wanajua.
[29.42] Kwa hakika Mwenyezi Mungu anajua kila kitu wanachokiomba badala yake Yeye. Na Yeye ndiye Mtukufu Mwenyenguvu Mwenye hikima.
[29.43] Na hiyo ni mifano tunawapigia watu, na hawaifahamuila wenye ilimu.
[29.44] Mwenyezi Mungu ameumba mbingu na ardhi kwa Haki.Kwa hakika katika hayo ipo Ishara kwa Waumini.
[29.45] SOMA uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala.Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwayakini kumdhukuru Mwenyezi Mungu ndilo jambo kubwa kabisa. Na Mwenyezi Mungu anayajua mnayoyatenda.
[29.46] Wala msijadiliane na Watu wa Kitabu ila kwa njiailiyo nzuri kabisa, isipo kuwa wale walio dhulumumiongoni mwao. Na semeni: Tumeyaamini yaliyo teremshwakwetu na yaliyo teremshwa kwenu. Na Mungu wetu naMungu wenu ni Mmoja. Na sisi ni wenye kusilimu kwake.
[29.47] Na namna hivi tumekuteremshia Kitabu (chaQur'ani). Basi wale tulio wapa Kitabu (cha Biblia)wataiamini (Qur'ani), na miongoni mwa hawa(washirikina) wapo watakao iamini. Na hawazikataiIshara zetu isipo kuwa makafiri.
[29.48] Na wewe hukuwa kabla yake unasoma kitabu chochote,wala hukukiandika kwa mkono wako wa kulia. Ingeli kuwahivyo wangeli fanya shaka wavunjifu.
[29.49] Bali hii (Qur'ani) ni Ishara zilizo wazi katikavifua vya walio pewa ilimu. Na hawazikatai Ishara zetuisipo kuwa wenye kudhulumu.
[29.50] Na walisema: Mbona hakuteremshiwa Ishara kutokakwa Mola wake Mlezi? Sema: Ishara ziko kwake MwenyeziMungu; ama mimi kwa hakika ni mwonyaji mwenye kubainisha tu.
[29.51] Je! Kwani hayakuwatosha ya kwamba tumekuteremshiaKitabu hiki wanacho somewa? Hakika katika hayo ziporehema na mawaidha kwa watu wanao amini.
[29.52] Sema: Mwenyezi Mungu anatosha kuwa ni Shahidibaina yangu na nyinyi. Anayajua yaliomo katika mbinguna ardhi. Na wale wanao amini upotovu na wakamkataa Mwenyezi Mungu, hao ndio walio khasiri.
[29.53] Na wanakuhimiza waletewe adhabu kwa haraka. Na laukuwa hapana wakati maalumu ulio wekwa, basi adhabuingeli wajia, na ingeli watokea kwa ghafla, na hali wao hawana khabari.
[29.54] Wanakuhimiza waletewe adhabu kwa haraka, na haliJahannamu kwa hakika imewazunguka makafiri!
[29.55] Siku itapo wafunika adhabu hiyo kutoka juu yao nachini ya miguu yao, na atasema: Onjeni hayo mliyo kuwamkiyatenda!
[29.56] Enyi waja wangu mlio amini! Kwa hakika ardhi yanguina wasaa. Basi niabuduni Mimi peke yangu.
[29.57] Kila nafsi itaonja mauti. Kisha mtarudishwa kwetu.
[29.58] Na ambao wameamini na wakatenda mema, bila yashaka tutawaweka katika maghorofa ya Peponi yenyekupitiwa chini yake mito, wakidumu humo. Ni mwema ulioje huo ujira wa watendao,
[29.59] Ambao walisubiri, na wakamtegemea Mola wao Mlezi.
[29.60] Na wanyama wangapi hawawezi kujimilikia rizikizao! Mwenyezi Mungu anawaruzuku hao na nyinyi pia. NaYeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
[29.61] Na ukiwauliza; Nani aliye umba mbingu na ardhi naakafanya jua na mwezi kuti'ii amri yake? Bila yashaka, watasema: Mwenyezi Mungu. Wapi basi wanako geuzwa?
[29.62] Mwenyezi Mungu humkunjulia, na humdhikishia,riziki amtakaye katika waja wake. Kwa hakika MwenyeziMungu ni Mjuzi wa kila kitu.
[29.63] Na ukiwauliza: Ni nani anaye teremsha maji kutokambinguni, na akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake?Bila ya shaka watasema: Ni Mwenyezi Mungu. Sema: Alhamdu Lillahi, Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu.Bali wengi katika wao hawafahamu.
[29.64] Na haya maisha ya dunia si chochote ila ni pumbaona mchezo. Na nyumba ya Akhera ndiyo maisha khasa;laiti wangeli kuwa wanajua!
[29.65] Na wanapo panda katika marikebu, humwomba MwenyeziMungu kwa kumsafia ut'iifu. Lakini anapo wavuawakafika nchi kavu, mara wanamshirikisha.
[29.66] Wapate kuyakanya tuliyo wapa, na wajistareheshe.Lakini watakuja jua!
[29.67] Je! Hawaoni ya kwamba tumeifanya nchi takatifu inaamani, na hali watu wengine wananyakuliwa kote kwamajirani zao? Je! Wanaamini upotovu, na neema za Mwenyezi Mungu wanazikataa?
[29.68] Na nani dhaalimu mkubwa kuliko yule anaye mzuliauwongo Mwenyezi Mungu au anaye kanusha Haki inapomjia? Je! Si katika Jahannamu ndio yatakuwa makaazi yamakafiri?
[29.69] Na wanao fanya juhudi kwa ajili yetu, Sisitutawaongoa kwenye njia zetu. Na hakika Mwenyezi Munguyu pamoja na watu wema.
Featured Ad
About Us
Contact Us
Advertise
Donate
Bookmark Us
Support Us
GuestBook
Link To Us
Newsletter
Recommend
Set as Home
Terms Of Use
What's New
Other Sites:
Know The Prophet campaign
-
Discover Islam
-
Pharmacy Site
-
Links SQL Plugins
This Page Was Last Updated on
Copyright 2003-2008
Islamic Education & Services Institute