Skip to Content
The Muslims Internet Directory
Featured Service
Home
-
FAQ
-
Forum
-
What's New
-
Shop
-
Million Pixels
-
Webmasters
-
Translate Me!
- Newsletter
-
Login/Register
Islamic Directory
Quran Tools
Hadith Tools
Islamic Library
Prayer Times
Discover Islam
Islamic Gallery
Classifieds
Free Services
Webmasters
Dictionary
Downloads
Shop!
Kids & Games
Quran Home
Multi Language Search
Translations
Transliteration
Quran Index
Chapter Info
English Search
Articles & Books
Audio
Audio Downloads
Memorization
Quran Links
On Your Site
FAQ
Muslims Internet Directory
The Quran / English
The Hadith
2Muslims.com
Our Network
Islamic Library & Articles
The Internet
Islamic Classifieds
WebRing Members Sites
Islamic Events Calendar
Islamic Forum
Options:
Advance
-
Live Search
-
Quran
-
Hadith
-
Search This Site
-
The Network
-
Forum
-
Classifieds
-
WebRing
-
Ajax
-
The Internet
-
Help!
Muslims Directory Google Gadgets
New
Prayer Times Worldwide
Featured Site
Discover Islam: Toward understanding Islam
Islam is probably the most misunderstood religion ...
:: Feature Your Site Now ::
Translate Site To:
Arabic
Chinese (Simplified)
French
German
Italian
Japanese
Korean
Portuguese
Spanish
Free Services
Muslims Million Pixels Advertising
Prayer Times Tables
Hadith Searchable Database
Submit an Article/Book
Submit an Event To Calendar
Free E-mail Account
Arabic/English Dictionary
Islamic IE Toolbar
Islamic Greeting Cards
Date Converter
FAQ About Islam
Islamic Male Names
Islamic Female Names
Zakat Calculator
Illusions: Tricks for the Eyes
Islamic Flashes
News Updates
Islamic Calendar 2006
How To Pray?
God's Attributes
Islamic Tests & Quizzes
Islamic CGI Scripts
Prayer Times Software
Print DAWA Tools
Vote Now!
Home
:
Quran:
Quran Translations:
Swahili:
SURAT AL I'MRAN :
Quran Translation and search engine in Swahili
Search the Quran in any of the drop down menu languages:
--Select language--
Albanian
Arabic
Azerbaijani
Bengali
Bosnian
Brazilian
Burmese
Chinese
Dutch
English_Abdullah_Yusuufali
English_Hasan_Qaribullah
English_Muhammad_Pickthall
Farsi
Finish
French
German
Hausa
Hindi
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latin
Malaysian
Melayu
Meranao
Mexican
Pashto
Persian
Poland
Portuguese
Russian
Spanish
Swahili
Tamil
Thai
Transliteration
Turkish
Urdu
More search options
SURAT AL I'MRAN
[3.1] Alif Laam Miim.
[3.2] Mwenyezi Mungu, hakuna mungu ila Yeye Aliye Hai,Msimamizi wa yote milele.
[3.3] Amekuteremshia Kitabu kwa haki, kinacho sadikishayaliyo kuwa kabla yake. Na aliteremsha Taurati naInjili
[3.4] Kabla yake, ziwe uwongofu kwa watu. Na akateremshaFurqani (Upambanuo). Hakika walio zikanusha Ishara zaMwenyezi Mungu watakuwa na adhabu kali. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye kulipa.
[3.5] Hakika Mwenyezi Mungu hakifichiki chochote kwake,duniani wala mbinguni.
[3.6] Yeye ndiye anaye kuundeni ndani ya matumbo yawazazi kwa namna apendayo. Hapana mungu ila Yeye,Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
[3.7]Yeye ndiye aliye kuteremshia Kitabu hichi. Ndaniyake zimo Aya muhkam, zenye maana wazi. Hizo ndizomsingi wa Kitabu hichi. Na ziko nyengine za mifano.Ama wale ambao nyoyoni mwao umo upotovu wanafuata zileza mifano kwa kutafuta fitna, na kutafuta maana yake;na wala hapana ajuaye maana yake ila Mwenyezi Mungu.Na wale wenye msingi madhubuti katika ilimu husema:Sisi tumeziamini, zote zimetoka kwa Mola wetu Mlezi.Lakini hawakumbuki hayo isipo kuwa wenye akili.
[3.8] (Na hao husema): Mola wetu Mlezi! Usizipotoe nyoyozetu baada ya kwisha tuongoa, na utupe rehema itokayokwako. Hakika Wewe ndiye Mpaji.
[3.9] Mola wetu Mlezi! Wewe ndiye Mkusanyaji wa watu kwaSiku isiyo na shaka ndani yake. Hakika Mwenyezi Munguhavunji miadi yake.
[3.10] Kwa hakika wale walio kufuru hazitowafaa kitu kwaMwenyezi Mungu mali zao, wala watoto wao; nao hao ndiokuni za Motoni-
[3.11] - Kama yaliyo wapata watu wa Firauni na wale waliokuwa kabla yao. Walikanusha Ishara zetu, basi MwenyeziMungu aliwashika kwa madhambi yao; na Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.
[3.12] Waambie walio kufuru: Karibuni mtashindwa namtakusanywa, mtiwe kwenye Jahannam; nako huko ni makaomabaya kabisa.
[3.13] Hakika ilikuwa ni Ishara kwenu katika yale majeshimawili yalipo pambana. Jeshi moja likipigana katikaNjia ya Mwenyezi Mungu, na jingine kafiri likiwaona zaidi kuliko wao mara mbili, kwa kuona kwa macho. NaMwenyezi Mungu humuunga mkono amtakaye kwa nusurayake. Hakika katika hayo yapo mazingatio kwa wenye macho.
[3.14] Watu wamepambiwa kupenda matamanio ya wanawake, nawana, na mirundi ya dhahabu na fedha, na farasi asili,na mifugo, na mashamba. Hayo ni starehe ya maisha ya duniani; na kwa Mwenyezi Mungu ndio kwenyemarejeo mema.
[3.15] Sema: Nikwambieni yaliyo bora kuliko hayo? Kwawachamngu ziko Bustani kwa Mola wao zipitazo mito katiyake. Watadumu humo, na wake walio takaswa, na wanazo radhi za Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu niMwenye kuwaona waja wake,
[3.16] Ambao husema: Mola wetu Mlezi! Hakika sisitumeamini, basi tufutie madhambi yetu, na tuepushe naadhabu ya Moto,
[3.17] Wanao subiri, wanao sema kweli, na wat'iifu, nawanao toa sadaka, na wanao omba maghafira kabla yaalfajiri.
[3.18] Mwenyezi Mungu, na Malaika, na wenye ilimu,wameshuhudia kuwa hakika hapana mungu ila Yeye, ndiyeMwenye kusimamisha uadilifu; hapana mungu ila YeyeMwenye nguvu na Mwenye hikima.17
[3.19] Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu niUislamu. Na walio pewa Kitabu hawakukhitalifiana ilabaada ya kuwajia ujuzi, kwa sababu ya uhasidi uliokuwa baina yao. Na anaye zikataa Ishara za MwenyeziMungu basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wakuhisabu.
[3.20] Na pindi wakikuhoji, basi sema: Miminimeusalimisha uso wangu kumwelekea Mwenyezi Mungu, nakadhaalika walio nifuata. Na waambie walio pewa Kitabuna wasio na kisomo: Je! Mmesilimu? Wakisilimu basiwameongoka. Na wakikengeuka basi juu yako ni kufikishaujumbe tu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaona wajawake.
[3.21] Hakika wanao zikataa Ishara za Mwenyezi Mungu, nawakawauwa Manabii pasipo haki, na wakawauwa watuwaamrishao Haki wabashirie adhabu kali.
[3.22] Hao ndio ambao vitendo vyao vimeharibika dunianina Akhera. Nao hawatapata wa kuwanusuru.
[3.23] Huwaoni wale walio pewa sehemu ya Kitabu? Wanaitwakukiendea Kitabu cha Mwenyezi Mungu ili kiwahukumubaina yao; kisha baadhi yao wanageuka wanakikataa.
[3.24] Hayo ni kwa sababu walisema: Hautatugusa Motoisipo kuwa kwa siku chache tu. Na yakawadanganyakatika dini yao yale ambayo wenyewe waliyo kuwawakiyazua.
[3.25] Basi itakuwaje tutakapo wakusanya Siku ambayohaina shaka kuja kwake? Na kila nafsi italipwa kamailivyo chuma, bila ya kudhulumiwa.
[3.26] Sema: Ewe Mwenyezi Mungu uliye miliki ufalme wote!Wewe humpa ufalme umtakaye, na humwondolea ufalmeumtakaye, na humtukuza umtakaye, na humuangusha umtakaye. Kheri yote iko mikononi mwako. Hakika Weweni Muweza wa kila kitu.
[3.27] Wewe huingiza usiku katika mchana, na huuingizamchana katika usiku. Na humtoa hai kutokana na maiti,na humtoa maiti kutokana na aliye hai. Na unamruzuku umtakaye bila ya hisabu.
[3.28] Waumini wasiwafanye makafiri kuwa wapenzi waobadala ya Waumini. Na anaye fanya hivyo, basi hatakuwachochote mbele ya Mwenyezi Mungu. Ila ikiwa kwa ajili ya kujilinda na shari zao. Na Mwenyezi Munguanakuhadharisheni naye. Na marejeo ni kwa MwenyeziMungu.
[3.29] Sema: Mkificha yaliyomo vifuani mwenu aumkiyafichua Mwenyezi Mungu anayajua; na anayajuayaliyomo mbinguni na yaliyomo duniani. Na MwenyeziMungu ni Muweza wa kila kitu.
[3.30] Siku ambayo kila nafsi itakuta mema iliyo yafanyayamehudhurishwa, na pia ubaya ilio ufanya. Itapendanafsi lau kungekuwako masafa marefu baina ya ubaya huo na yeye. Na Mwenyezi Mungu anakuhadharisheni naye.Na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja wake.
[3.31] Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basinifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni naatakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu niMwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu.
[3.32] Sema: Mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume. Nawakigeuka basi Mwenyezi Mungu hawapendi makafiri.
[3.33] Hakika Mwenyezi Mungu alimteuwa Adam na Nuhu naukoo wa Ibrahim na ukoo wa Imran juu ya walimwenguwote.
[3.34] Ni wazao wao kwa wao; na Mwenyezi Mungu ni Mwenyekusikia na Mwenye kujua.
[3.35] Alipo sema mke wa Imran: Mola wangu Mlezi!Nimekuwekea nadhiri kilichomo tumboni mwangu kuwawakfu; basi nikubalie. Hakika Wewe ndiye Mwenyekusikia na Mwenye kujua.
[3.36] Basi alipo mzaa alisema: Mola wangu Mlezi!Nimemzaa mwanamke - na Mwenyezi Mungu anajua sanaaliye mzaa - Na mwanamume si sawa na mwanamke. Na miminimemwita Maryamu. Nami namkinga kwako, yeye na uzaowake, uwalinde na Shet'ani aliye laaniwa.
[3.37] Tena Mola wake Mlezi akampokea kwa mapokeo mema naakamkuza makuzo mema, na akamfanya Zakariya awe mleziwake. Kila mara Zakariya alipo ingia chumbani kwake alimkuta na vyakula. Basi alimwambia: Ewe Maryamu!Unavipata wapi hivi? Naye akasema: Hivi vinatoka kwaMwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hisabu.
[3.38] Pale pale Zakariya akamwomba Mola wake Mlezi,akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe kutoka kwako uzaomwema. Wewe ndiye unaye sikia maombi.
[3.39] Alipo kuwa kasimama chumbani akisali, Malaikakamnadia: Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria Yahya,ataye kuwa mwenye kusadikisha neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu, na ni bwana na mt'awa na Nabii kwawatu wema.
[3.40] Akasema Zakariya: Mola wangu Mlezi! Vipi nitapatamwana na hali ukongwe umenifikia, na mke wangu nitasa? Akasema: Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu hufanya apendavyo.
[3.41] Akasema: Mola wangu Mlezi! Niwekee alama. Akasema:Alama yako ni kuwa hutasema na watu kwa siku tatu,isipo kuwa kwa kuashiria tu. Na mdhukuru Mola Mlezi wako kwa wingi na mtakase jioni na asubuhi.
[3.42] Na angalia pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu!Kwa hakika Mwenyezi Mungu amekuteuwa, na akakutakasa,na akakutukuza kuliko wanawake wote.
[3.43] Ewe Maryamu! Mnyenyekee Mola Mlezi wako na usujuduna uiname pamoja na wainamao.
[3.44] Hizi ni khabari za ghaibu tunazo kufunulia; nawehukuwa nao walipo kuwa wakitupa kalamu zao nani waoatamlea Maryamu, na hukuwa nao walipo kuwa wakishindana.
[3.45] Na pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! HakikaMwenyezi Mungu anakubashiria (mwana) kwa neno litokalokwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, namiongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu).
[3.46] Naye atazungumza na watu katika utoto wake nakatika utuuzima wake, na atakuwa katika watu wema.
[3.47] Maryamu akasema: Mola wangu Mlezi! Vipi nitampatamwana na hali hajanigusa mwanaadamu? Mwenyezi Munguakasema: Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu huumba apendacho. Anapo hukumu jambo, huliambia: Kuwa!Likawa.
[3.48] Na atamfunza kuandika na Hikima na Taurati naInjili.
[3.49] Na ni Mtume kwa Wana wa Israili kuwaambia: Miminimekujieni na Ishara kutoka kwa Mola Mlezi wenu, yakwamba nakuundieni kwa udongo kama sura ya ndege.Kisha nampuliza anakuwa ndege kwa idhini ya MwenyeziMungu. Na ninawaponesha vipofu wa tangu kuzaliwa nawakoma, na ninawafufua maiti kwa idhini ya MwenyeziMungu, na ninakwambieni mnacho kila na mnacho wekaakiba katika nyumba zenu. Hakika katika haya ipo Ishara kwenu ikiwi nyinyi ni wenye kuamini.
[3.50] Na ninasadikisha yaliyo kuwa kabla yangu katikaTaurati, na ili nikuhalalishieni baadhi ya yale mlioharimishiwa, na nimekujieni na Ishara kutokana na Mola Mlezi wenu. Kwa hivyo mcheni MwenyeziMungu na nit'iini mimi.
[3.51] Hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi na niMola wenu Mlezi. Basi muabudni Yeye. Hii ndiyo NjiaIliyo Nyooka.
[3.52] Isa alipo hisi kuwa kati yao pana ukafiri alisema:Nani wasaidizi wangu kwa Mwenyezi Mungu? Wanafunziwake wakasema: Sisi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu. Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na shuhudia kwamba sisihakika ni Waislamu.
[3.53] Mola wetu Mlezi! Tumeyaamini uliyo yateremsha, natumemfuata huyu Mtume, basi tuandike pamoja na wanaoshuhudia.
[3.54] Na Makafiri walipanga mipango na Mwenyezi Munguakapanga mipango, na Mwenyezi Mungu ndiye mbora wawenye kupanga.
[3.55] Pale Mwenyezi Mungu alipo sema: Ewe Isa! Miminitakufisha, na nitakunyanyua kwangu, na nitakutakasana wale walio kufuru, na nitawaweka wale walio kufuatajuu ya wale walio kufuru, mpaka Siku ya Kiyama. Kishamarejeo yenu yatakuwa kwangu, nikuhukumuni katika yalemliyo kuwa mkikhitalifiana.
[3.56] Ama wale walio kufuru, nitawaadhibu adhabu kalikatika dunia na Akhera, wala hawatapata wa kuwanusuru.
[3.57] Na ama wale walio amini na wakatenda mema basiMwenyezi Mungu atawalipa ujira wao kaamili. NaMwenyezi Mungu hawapendi madhaalimu.
[3.58] Haya tunayo kusomea ni katika Aya na Ukumbushowenye hikima.
[3.59] Hakika mfano wa Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kamamfano wa Adam; alimuumba kwa udongo kisha akamwambia:Kuwa! Basi akawa.
[3.60] Hii ni kweli itokayo kwa Mola wako Mlezi. Basiusiwe miongoni mwa wanao fanya shaka.
[3.61] Watakao kuhoji katika haya baada ya kukufikiliailimu hii waambie: Njooni tuwaite watoto wetu nawatoto wenu, na wake zetu na wake zenu, na sisiwenyewe na nyinyi wenyewe, kisha tuombe kwaunyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.
[3.62] Hakika haya ndiyo maelezo ya kweli. Na hakunamungu ila Mwenyezi Mungu tu, na hakika Mwenyezi Mungundiye Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
[3.63] Na kama wakigeuka basi Mwenyezi Mungu anawajuawaharibifu.
[3.64] Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye nenolilio sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabuduyeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa WaolaWalezi badala ya Mwenyezi Mungu. Na wakigeuka basisemeni: Shuhudi- eni ya kwamba sisi ni Waislamu.
[3.65] Enyi Watu wa Kitabu! Mbona mnabishana juu yaIbrahim, na hali Taurati na Injili hazikuteremshwa ilabaada yake? Basi hamzingatii?
[3.66] Angalieni! Nyinyi mlibishana katika yale mliyoyajua. Mbona sasa mnabishana katika yale msiyo yajua?Na Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye, na nyinyi hamjui.
[3.67] Ibrahim hakuwa Yahudi wala Mkristo, lakini alikuwamwongofu Muislamu, wala hakuwa katika washirikina.
[3.68] Watu wanao mkaribia zaidi Ibrahim ni wale waliomfuata yeye na Nabii huyu na walio amini. Na MwenyeziMungu ndiye Mlinzi wa Waumini.
[3.69] Kipo kikundi katika Watu wa Kitabu wanao pendakukupotezeni; lakini hawapotezi ila nafsi zao, naowenyewe hawatambui.
[3.70] Enyi Watu wa Kitabu! Mbona mnazikataa Ishara zaMwenyezi Mungu ilhali nyinyi mnashuhudia?
[3.71] Enyi Watu wa Kitabu! Mbona kweli mnaivisha uwongo,na kweli mnaificha na hali mnajua?
[3.72] Na kikundi katika Watu wa Kitabu walisema:Yaaminini yale waliyo teremshiwa wenye kuamini mwanzowa mchana, na yakataeni mwisho wake; huenda wakarejea.
[3.73] Wala msimuamini ila anaye fuata dini yenu. Sema:Hakika uwongofu ni uwongofu wa Mwenyezi Mungu, kuwaapewe mtu mfano wa mlio pewa nyinyi au wakuhojinimbele ya Mola wenu Mlezi. Sema: Hakika fadhila zimomikononi mwa Mwenyezi Mungu. Humpa amtakaye. NaMwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa na Mjuzi.
[3.74] Yeye humchagua kumpa rehema zake amtakaye; naMwenyezi Mungu ndiye Mwenye fadhila kubwa.
[3.75] Na miongoni mwa Watu wa Kitabu yupo ambaye ukimpaamana ya mrundi wa mali atakurudishia, na miongonimwao yupo ambaye ukimpa amana ya dinari moja hakurudishii isipo kuwa ukimsimamia kumdai. Haya nikwa kuwa wakisema: Hatuna lawama kwa ajili ya hawawasio jua kusoma. Na wanamzulia uwongo Mwenyezi Mungu,hali nao wanajua.
[3.76] Sivyo hivyo, bali anaye timiza ahadi yake naakamchamngu basi Mwenyezi Mungu huwapenda wachamngu.
[3.77] Hakika wanao uza ahadi ya Mwenyezi Mungu na viapovyao thamani ndogo, hao hawatakuwa na sehemu ya kheriyoyote katika Akhera, wala Mwenyezi Mungu hatasema nao wala hatawatazama Siku ya Kiyama, walahatawatakasa, nao watapata adhabu chungu.
[3.78] Na wapo baadhi yao wanao pindua ndimi zao katikakusoma Kitabu ili mdhanie kuwa hayo yanatoka Kitabuni,na wala hayatoki Kitabuni. Na husema: Haya yametoka kwa Mwenyezi Mungu. Na wala hayatoki kwa MwenyeziMungu. Na wanamsingizia Mwenyezi Mungu uwongo na waowanajua.
[3.79] Haiwezi kuwa mtu aliye pewa na Mwenyezi MunguKitabu na hikima na Unabii kisha awaambie watu: Kuweniwa kuniabudu mimi badala ya Mwenyezi Mungu. Bali atawaambia: Kuweni wenye kumuabudu Mola Mlezi waviumbe vyote, kwa kuwa nyinyi mnafundisha Kitabu nakwa kuwa mnakisoma.
[3.80] Wala hatakuamrisheni kuwafanya Malaika na Manabiikuwa ni miungu. Je, atakuamrisheni ukafiri baada yakuwa nyinyi Waislamu?
[3.81] Na pale Mwenyezi Mungu alipo chukua ahadi kwaManabii: Nikisha kupeni Kitabu na hikima, kishaakakujieni Mtume mwenye kusadikisha mliyo nayo, ni juuyenu mumuamini na mumsaidie. Akasema: Je, mmekiri nammekubali kushika agizo langu juu ya hayo? Wakasema:Tumekubali. Akasema: Basi shuhudieni, na Mimi nipamoja nanyi katika kushuhudia.
[3.82] Watakao geuka baada ya haya basi hao ndiowapotovu.
[3.83] Je, wanataka dini isiyo kuwa ya Mwenyezi Mungu, nahali kila kilichomo mbinguni na katika ardhikimesilimu kwa kumt'ii Yeye kikipenda kisipende, na kwake Yeye watarejeshwa?
[3.84] Sema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na tuliyoteremshiwa sisi, na aliyo teremshiwa Ibrahim, naIsmail, na Is-haak na Yaakub na wajukuu zao, na aliyo pewa Musa na Isa na Manabii wengine kutoka kwa Molawao Mlezi. Hatubagui baina yao hata mmoja, na sisi niwenye kusilimu kwake.
[3.85] Na anaye tafuta dini isiyo kuwa Uislamuhaitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenyekukhasiri.
[3.86]Mwenyezi Mungu atawaongoaje watu walio kufuru baadaya kuamini kwao, na wakashuhudia ya kuwa Mtume huyu niwa haki, na zikawafikia hoja zilizo wazi? Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhaalimu.
[3.87] Hao malipo yao ni kuwa ipo juu yao laana yaMwenyezi Mungu na ya Malaika na ya watu wote.
[3.88] Humo watadumu. Hawatapunguziwa adhabu walahawatapewa nafasi.
[3.89] Isipo kuwa wale walio tubu baada ya hayo nawakatengenea; kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehena Mwenye kurehemu.
[3.90] Hakika wale walio kufuru baada ya kuamini kwao,kisha wakazidi kukufuru, toba yao haitakubaliwa, nahao ndio walio potea.
[3.91] Hakika wale walio kufuru, na wakafa hali nimakafiri haitakubaliwa kutoka kwa yeyote wao fidia yadhahabu ya kujaza dunia nzima lau wangeli itoa. Hao watapata adhabu chungu, wala hawatakuwa na wakuwanusuru.
[3.92] KABISA HAMTAFIKIA wema mpaka mtoe katika vilemnavyo vipenda. Na kitu chochote mnacho kitoa basihakika Mwenyezi Mungu anakijua.
[3.93] Kila chakula kilikuwa halali kwa Wana wa Israiliisipo kuwa alicho jizuilia Israili mwenyewe kablahaijateremshwa Taurati. Sema: Leteni Taurati muisome ikiwa nyinyi ni wasema kweli.
[3.94] Na wanao mzulia uwongo Mwenyezi Mungu baada yahayo, basi hao ndio madhaalimu.
[3.95] Sema: Mwenyezi Mungu amesema kweli. Basi fuatenimila ya Ibrahim mwongofu, wala hakuwa miongoni mwawashirikina.
[3.96] Hakika Nyumba ya kwanza walio wekewa watu kwaibada ni ile iliyoko Bakka, iliyo barikiwa na yenyeuwongofu kwa walimwengu wote.
[3.97] Ndani yake zipo Ishara zilizo wazi - masimamio yaIbrahim, na mwenye kuingia humo anakuwa katika amani.Na kwa ajili ya Mwenyezi Mungu imewajibikia watu wahiji kwenye Nyumba hiyo, kwa yule awezae njia yakwendea. Na atakaye kanusha basi Mwenyezi Mungu simhitaji kwa walimwengu.
[3.98] Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Kwa nini mnakanushaishara za Mwenyezi Mungu, na ilhali kuwa MwenyeziMungu ni Shahidi kwa yote mnayo yatenda?
[3.99] Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Kwa nini mnamzuiliaaliye amini Njia ya Mwenyezi Mungu mkiitafutia kosa,na hali nyinyi mnashuhudia? Na Mwenyezi Mungu simwenye kughafilika na mnayo yatenda.
[3.100] Enyi mlio amini! Mkiwat'ii baadhi ya walio pewaKitabu watakurudisheni kuwa makafiri baada ya Imaniyenu.
[3.101] Na vipi mkufuru hali nyinyi mnasomewa Aya zaMwenyezi Mungu na Mtume yuko kati yenu? Na mwenyekushikamana na Mwenyezi Mungu basi huyo ameongozwakwenye Njia Iliyo Nyooka.
[3.102] Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu kamaipasavyo kumcha; wala msife ila nanyi ni Waislamu.
[3.103] Na shikamaneni kwa Kamba ya Mwenyezi Mungu nyotepamoja, wala msifarikiane. Na kumbukeni neema yaMwenyezi Mungu iliyo juu yenu: vile mlivyo kuwa nyinyikwa nyinyi maadui naye akaziunganisha nyoyo zenu; kwaneema yake mkawa ndugu. Na mlikuwa ukingoni mwa shimola Moto, naye akakuokoeni nalo. Namna hivi Mwenyezi Mungu anakubainishieni Ishara zake ili mpate kuongoka.
[3.104] Na uwe kutokana na nyinyi umma unao linganiakheri na unao amrisha mema na unakataza maovu. Na haondio walio fanikiwa.
[3.105] Wala msiwe kama wale walio farikiana nakukhitalifiana baada ya kuwafikia hoja zilizo wazi. Nahao ndio watakao kuwa na adhabu kubwa.
[3.106] Siku ambayo nyuso zitanawiri na nyusozitasawijika. Ama hao ambao nyuso zao zitasawijika wataambiwa: Je! Mlikufuru baada yakuamini kwenu? Basi onjeni adhabu kwa vile mlivyo kuwamnakufuru.
[3.107] Ama wale ambao nyuso zao zitanawiri watakuwakatika rehema ya Mwenyezi Mungu. Wao humo watadumu.
[3.108] Hizi ni Aya za Mwenyezi Mungu tunakusomea kwahaki. Na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu walimwengu.
[3.109] Na kila kilichomo mbinguni na kilichomo ardhinini cha Mwenyezi Mungu; na mambo yote yatarejea kwaMwenyezi Mungu.
[3.110] Nyinyi mmekuwa bora ya umma walio tolewa watu,kwa kuwa mnaamrisha mema na mnakataza maovu, namnamuamini Mwenyezi Mungu. Na lau kuwa Watu wa Kitabunao wameamini ingeli kuwa bora kwao. Wapo miongonimwao waumini, lakini wengi wao wapotovu.
[3.111] Maadui hawatakudhuruni ila ni maudhi tu. Nawakipigana nanyi watakupeni mgongo, na tenahawatanusuriwa.
[3.112] Wamepigwa na udhalili popote wanapo kutikana,isipo kuwa wakishika kamba ya Mwenyezi Mungu na kambaya watu. Na wakastahiki ghadhabu ya Mwenyezi Mungu, nawamepigwa na unyonge. Hayo ni kwa sababu walikuwawakizikataa Ishara za Mwenyezi Mungu, na wakiwauwaManabii pasina haki; hayo ni kwa sababu waliasi nawalikuwa wakiruka mipaka.
[3.113] Wote hao si sawa sawa. Miongoni mwa Watu waKitabu wamo watu walio simama baraabara, wanasoma Ayaza Mwenyezi Mungu nyakati za usiku, na pia wanasujudu.
[3.114] Wanamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, nawanaamrisha mema na wanakataza maovu na wanakimbiliakatika mambo ya kheri. Na hao ndio miongoni mwa watenda mema.
[3.115] Na kheri yoyote wanayo ifanya hawatanyimwamalipwa yake. Na Mwenyezi Mungu anawajua wachamngu.
[3.116] Hakika wale walio kufuru hazitawafaa kitu malizao wala watoto wao mbele ya Mwenyezi Mungu. Na haondio watu wa Motoni - humo watadumu.
[3.117] Mfano wa vile wanavyo vitoa katika uhai wao waduniani ni kama upepo ambao ndani yake ipo baridi yabarafu, ukalisibu shamba la watu walio dhulumu nafsi zao, ukaliteketeza. Na Mwenyezi Mungu hakuwadhulumu,bali wao wenyewe wanadhulumu nafsi zao.
[3.118] Enyi mlio amini! Msiwafanye wasiri wenu watuwasio kuwa katika nyinyi. Hawataacha kukufanyieniubaya. Wanayapenda yanayo kudhuruni. Imekwisha fichukachuki yao katika midomo yao. Na yanayo ficha vifuavyao ni makubwa zaidi. Tumekwisha kubainishieni Isharaikiwa nyinyi mtayatia akilini.
[3.119] Hivyo basi nyinyi ndio mnawapenda watu hao, walawao hawakupendeni. Nanyi mnaviamini Vitabu vyote. Nawanapo kutana nanyi husema: Tumeamini. Na wanapo kuwa peke yao wanakuumieni vidole kwa chuki. Sema:Kufeni kwa chuki yenu! Hakika Mwenyezi Mungu anayajuayaliomo vifuani.
[3.120] Ikikupateni kheri huwaudhi. Na ikikupateni shariwanafurahia. Na nyinyi mkisubiri na mkajizuilia, hilazao hazitakudhuruni kitu. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kuyazunguka yote wayatendayo.
[3.121] Na pale ulipo toka asubuhi, ukaacha ahali zakouwapange Waumini kwenye vituo kwa ajili ya vita - naMwenyezi Mungu anasikia na anajua.
[3.122] Makundi mawili miongoni mwenu yakaingiwa na wogakuwa watashindwa - na hali Mwenyezi Mungu ndiye Mlinziwao; na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu.
[3.123] Na Mwenyezi Mungu alikwisha kunusuruni katikaBadri nanyi mlikuwa wanyonge. Basi mcheni MwenyeziMungu ili mpate kushukuru.
[3.124] Ulipo waambia Waumini: Je, haitakutosheni ikiwaMola wenu atakusaidieni kwa Malaika elfu tatu walioteremshwa?
[3.125] Kwani! Ikiwa mtavumilia na mkamchamngu na hatamaadui wakikutokeeni kwa ghafla, basi hapo Mola wenuMlezi atakusaidieni kwa Malaika elfu tano wanao shambulia kwa nguvu.
[3.126] Na Mwenyezi Mungu hakufanya haya ila kuwa nibishara kwenu, na ili nyoyo zenu zipate kutua. Namsaada hautoki isipo kuwa kwa Mwenyezi Mungu, Aliye tukuka, Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
[3.127] Haya ni kwa ajili awakate sehemu katika waliokufuru, au awahizi wapate kurejea nyuma naowamepwelewa.
[3.128] Wewe huna lako jambo katika haya - amaatawahurumia au atawaadhibu, kwani wao ni madhaalimu.
[3.129] Na ni vya Mwenyezi Mungu vyote vilivyomo katikambingu na vilivyomo katika ardhi. Yeye humsamehe nahumuadhibu amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Msamehevu Mwenye kurehemu.
[3.130] Enyi mlio amini! Msile riba mkizidisha juu kwajuu, na mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kufanikiwa.
[3.131] Na uogopeni Moto ambao umeandaliwa kwa ajili yamakafiri.
[3.132] Na mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume ili mpatekurehemewa.
[3.133] Na yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi, naPepo ambayo upana wake ni mbingu na ardhi, iliyo wekwatayari kwa wachamngu,
[3.134] Ambao hutoa wanapo kuwa na wasaa na wanapo kuwana dhiki, na wanajizuia ghadhabu, na wasamehevu kwawatu; na Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao wema;
[3.135] Na ambao pindi wafanyapo uchafu au wakajidhulumunafsi zao humkumbuka Mwenyezi Mungu na wakamwombamsamaha kwa dhambi zao - na nani anaye futa dhambi isipo kuwa Mwenyezi Mungu? - na wala hawaendelei nawaliyo yafanya na hali wanajua.
[3.136] Hao malipo yao ni msamaha kwa Mola wao Mlezi, naBustani zipitazo mito kati yake. Humo watadumu, namwema mno ujira wa watendao.
[3.137] Kabla yenu zimepita nyendo nyingi; basi tembeenikatika ulimwengu muangalie vipi ulikuwa mwisho wawanao kanusha.
[3.138] Hii ni bayana kwa watu wote, na ni uwongofu, namawaidha kwa wachamngu.
[3.139] Wala msilegee, wala msihuzunike, kwani nyinyindio wa juu mkiwa ni Waumini.
[3.140] Kama yamekupateni majaraha, basi na hao watuwengine yamewapata majaraha mfano wa haya. Na siku zanamna hii tunaweletea watu kwa zamu, ili Mwenyezi Mungu awapambanue walio amini na awateuwe miongonimwenu mashahidi. Na Mwenyezi Mungu hawapendimadhaalimu;
[3.141] Na pia ili Mwenyezi Mungu awasafishe walio aminina awafutilie mbali makafiri.
[3.142] Je! Mnadhani mtaingia Peponi na hali MwenyeziMungu hajawapambanua wale miongoni mwenu walio piganaJihadi, na hajawapambanua walio subiri?
[3.143] Na nyinyi mlikuwa mkitamani mauti kablahamjakutana nayo. Basi sasa mmekwisha yaona na hukumnayatazama.
[3.144] Na Muhammad hakuwa ila ni Mtume tu. Wamekwishapita kabla yake Mitume. Je, akifa au akauwawa ndiyomtageuka mrudi nyuma? Na atakaye geuka akarudi nyuma huyo hatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Munguatawalipa wanao mshukuru.
[3.145] Na haiwezi nafsi kuwa ife ila kwa idhini yaMwenyezi Mungu kama ilivyo andikwa ajali yake. Namwenye kutaka malipo ya duniani tutampa; na mwenyekutaka malipo ya Akhera tutampa. Na tutawalipa wenyekushukuru.
[3.146] Na Manabii wangapi walipigana na pamoja naoWaumini wengi wenye ikhlasi! Hawakufanya woga kwayaliyo wasibu katika Njia ya Mwenyezi Mungu, wala hawakudhoofika wala hawakuwa wanyonge. Na MwenyeziMungu huwapenda wanao subiri.
[3.147] Wala kauli yao haikuwa ila ni kusema: Mola wetuMlezi! Tughufirie madhambi yetu na kupita kwetu kiasikatika mambo yetu, na isimamishe imara miguu yetu na utunusuru tuwashinde kaumu ya makafiri.
[3.148] Basi Mwenyezi Mungu akawapa malipo ya duniani nabora ya malipo ya Akhera. Na Mwenyezi Mungu anawapendawafanyao mema.
[3.149] Enyi mlio amini! Ikiwa mtawat'ii walio kufuruwatakurudisheni nyuma, na hapo mtageuka kuwa wenyekukhasiri.
[3.150] Bali Mwenyezi Mungu ndiye Mlinzi wenu, naye ndiyebora wa wasaidizi.
[3.151] Tutazitia khofu nyoyo za walio kufuru kwa vilewalivyo mshirikisha Mwenyezi Mungu na washirika ambaohakuwateremshia hoja yoyote. Na makaazi yao ni Motoni;na maovu yaliyoje maskani ya wenye kudhulumu!
[3.152] Na Mwenyezi Mungu alikutimilizieni miadi yake,vile mlivyo kuwa mnawauwa kwa idhini yake, mpaka mlipolegea na mkazozana juu ya amri, na mkaasi baada ya Yeye kukuonyesheni mliyo yapenda. Wapo miongoni mwenuwanao taka dunia, na wapo miongoni mwenu wanao takaAkhera. Kisha akakutengeni nao (maadui) ili akujaribuni. Naye sasa amekwisha kusameheni. NaMwenyezi Mungu ni Mwenye fadhila juu ya Waumini.
[3.153] Pale mlipo kuwa mkikimbia mbio wala hamumsikiliziyeyote, na Mtume anakuiteni, yuko nyuma yenu. MwenyeziMungu akakupeni dhiki juu ya dhiki, ili msisikitike kwa yaliyo kukoseeni wala kwa yaliyokusibuni. Na Mwenyezi Mungu anazo khabari za yotemnayo yatenda.
[3.154] Kisha baada ya dhiki alikuteremshieni utulivu -usingizi ambao ulifunika kundi moja kati yenu. Nakundi jengine nafsi zao ziliwashughulisha hata wakamdhania Mwenyezi Mungu dhana isiyo kuwa ya haki,dhana ya kijinga. Wakisema: Hivyo tuna lolote sisikatika jambo hili? Sema: Mambo yote ni ya MwenyeziMungu. Wanaficha katika nafsi zao wasiyo kubainishia.Wanasema: Lau ingelikuwa tuna lolote katika jambo hilitusinge uliwa hapa. Sema: Hata mngeli kuwa majumbani mwenu, basi wangeli toka walio andikiwa kufa, wakendamahali pao pa kuangukia wafe.(Haya ni hivyo) iliMwenyezi Mungu ayajaribu yaliyomo vifuani mwenu, na asafishe yaliyomo nyoyoni mwenu. Na Mwenyezi Munguanayajua yaliyomo vifuani.
[3.155] Hakika wale walio rudi nyuma miongoni mwenu sikuyalipo pambana majeshi mawili, Shet'ani ndiye aliyewatelezesha kwa sababu ya baadhi ya makosa waliyo yafanya; na Mwenyezi Mungu amekwisha wasamehe. HakikaMwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mpole.
[3.156] Enyi mlio amini! Msiwe kama wale walio kufuru nawakawasema ndugu zao walipo safiri katika nchi auwalipo kuwa vitani: Wangeli kuwa kwetu wasingeli kufa na wasingeli uwawa. Ili Mwenyezi Mungu afanyehayo kuwa ni majuto katika nyoyo zao. Na MwenyeziMungu huhuisha na hufisha. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenyekuyaona myatendayo.
[3.157] Na pindi mkiuliwa katika Njia ya Mwenyezi Mungu,au mkifa, hakika maghfira na rehema zitokazo kwaMwenyezi Mungu ni bora kuliko yote wanayo yakusanya.
[3.158] Na mkifa au mkiuliwa ni kwa Mwenyezi Mungu ndiomtakusanywa.
[3.159] Basi ni kwa sababu ya rehema itokayo kwa MwenyeziMungu ndio umekuwa laini kwao. Na lau ungeli kuwamkali, mwenye moyo mgumu, bila ya shaka wangeli kukimbia. Basi wasamehe, na waombee maghfira, nashauriana nao katika mambo. Na ukisha kata shauri basimtegemee Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Munguhuwapenda wanao mtegemea.
[3.160] Akikunusuruni Mwenyezi Mungu hapana wakukushindeni, na akikutupeni ni nani, basi, baada yakeYeye ataye kunusuruni? Na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu.
[3.161] Na haiwezekani kwa Nabii yeyote kufanya khiyana.Na atakaye fanya khiyana, atayaleta Siku ya Kiyamaaliyo yafanyia khiyana, kisha kila mtu atalipwa kwa aliyo yachuma, kwa ukamilifu; wala hawatadhulumiwa.
[3.162] Je! Aliye yafuata ya kumridhisha Mwenyezi Mungini kama yule aliye stahiki ghadhabu ya Mwenyezi Mungu,na makaazi yake yakawa Jahannamu? Napo ni mahala pabaya pa kurejea.
[3.163] Hao wana vyeo mbali mbali kwa Mwenyezi Mungu. NaMwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona yote wayatendayo.
[3.164] Hakika Mwenyezi Mungu amewafanyia wema mkubwaWaumini vile alivyo waletea Mtume aliye miongoni mwaowenyewe, anaye wasomea Aya zake, na anawatakasa, na anawafunza Kitabu na hikima, ijapo kuwa kabla ya hapowalikuwa katika upotovu ulio wazi.
[3.165] Nyinyi - ulipo kusibuni msiba ambao nyinyimmekwisha watia mara mbili mfano wa huo - mnasema:Umetoka wapi huu? Sema: Huo umetoka kwenu wenyewe.Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye uweza juu ya kilakitu.
[3.166] Na yaliyo kusibuni siku yalipo pambana majeshimawili yalikuwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na iliawajue Waumini.
[3.167] Na ili awapambanue walio kuwa wanaafiki,wakaambiwa: Njooni mpigane katika Njia ya MwenyeziMungu au lindeni. Wakasema: Tungeli jua kuna kupiganabila ya shaka tungeli kufuateni. Wao siku ile walikuwakaribu na ukafiri kuliko Imani. Wanasema kwa midomoyao yasiyo kuwamo nyoyoni mwao. Na Mwenyezi Munguanajua kabisa wanayo yaficha.
[3.168] Hao ndio walio waambia ndugu zao na wao wenyewewakakaa kitako: Lau wengeli tut'ii wasingeli uliwa.Sema: Ziondoleeni nafsi zenu mauti kama mnasema kweli.
[3.169] Wala kabisa usiwadhanie walio uliwa katika Njiaya Mwenyezi Mungu kuwa ni maiti. Bali hao ni wahai,wanaruzukiwa kwa Mola wao Mlezi.
[3.170] Wanafurahia aliyo wapa Mwenyezi Mungu kwa fadhilayake, na wanawashangilia wale ambao bado hawajajiunganao, walio nyuma yao, ya kwamba haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika.
[3.171] Wanashangilia neema na fadhila za Mwenyezi Mungu,na ya kwamba Mwenyezi Mungu hapotezi ujira wa Waumini,
[3.172] Walio mwitikia Mwenyezi Mungu na Mtume baada yakwisha patwa na majaraha - kwa walio fanya wemamiongoni mwao na wakamchamngu utakuwa ujira mkubwa -
[3.173] Walio ambiwa na watu: Kuna watuwamekukusanyikieni, waogopeni! Hayo yakawazidishiaImani, wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosha, naye nimbora wa kutegemewa.
[3.174] Basi wakarudi na neema na fadhila za MwenyeziMungu. Hapana baya lilio wagusa, na wakafuata yanayomridhi Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye fadhila kuu.
[3.175] Hakika huyo ni Shet'ani anawatia khofu marafikizake, basi msiwaogope, bali niogopeni Mimi mkiwanyinyi ni Waumini.
[3.176] Wala wasikuhuzunishe wale wanao kimbiliaukafirini. Hakika hao hawamdhuru kitu Mwenyezi Mungu.Mwenyezi Mungu anataka asiwawekee sehemu yoyote katikaAkhera, na yao wao adhabu kubwa.
[3.177] Hakika wale walio nunua ukafiri kwa Imanihawatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu, na yao wao ni adhabuchungu.
[3.178] Wala wasidhani wale wanao kufuru kwamba huumuhula tunao wapa ni kheri yao. Hakika tunawapa muhulawazidi madhambi. Na yao wao ni adhabu yakuwadhalilisha.
[3.179] Haiwi kwa Mwenyezi Mungu kuwaacha Waumini katikahali mliyo nayo mpaka apambanue wabaya na wema. Walahaiwi kwa Mwenyezi Mungu kukujuulisheni mambo ya ghaibu. Lakini Mwenyezi Mungu humteua katika Mitumewake amtakaye. Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mitumeyake. Na mkiamini na mkamchamngu mtakuwa na ujira mkubwa.
[3.180] Wala wasidhani wale ambao wanafanya ubakhilikatika aliyo wapa Mwenyezi Mungu katika fadhila zakekuwa ni kheri yao. Bali hiyo ni shari kwao. Watafungwakongwa za yale waliyo yafanyia ubakhili Siku yaKiyama. Na urithi wa mbingu na ardhi ni wa MwenyeziMungu. Na Mwenyezi Mungu anazo khabari za yotemyatendayo.
[3.181] Mwenyezi Mungu amekwisha sikia kauli ya waliosema: Mwenyezi Mungu ni masikini, na sisi ni matajiri.Tumeyaandika waliyo yasema, na pia kuwauwa kwao Manabii bila ya haki, na tutawaambia Siku ya Kiyama:Onjeni adhabu ya kuungua.
[3.182] Haya ni kwa sababu ya iliyo tanguliza mikonoyenu, na kwamba Mwenyezi Mungu si mwenye kuwadhulumuwaja,
[3.183] Walio sema: Mwenyezi Mungu ametuahidi tusimuaminiMtume yeyote mpaka atuletee kafara inayo teketezwa namoto. Waambie: Walikujieni Mitume kabla yangu kwa hoja zilizo wazi na kwa hayo mnayo sema, basi kwanini mkawauwa ikiwa mlikuwa wakweli?
[3.184] Na wakikukanusha basi walikanushwa Mitume wenginekabla yako walio kuja na hoja waziwazi na Vitabuvyenye hikima, na Kitabu chenye nuru.
[3.185] Kila nafsi itaonja mauti. Na bila ya shakamtapewa ujira wenu kaamili Siku ya Kiyama. Na atakayeepushwa na Moto na akatiwa Peponi basi huyo amefuzu.Na maisha ya dunia si kitu ila ni starehe yaudanganyifu.
[3.186] Hapana shaka yoyote mtapata misukosuko katikamali zenu na nafsi zenu, na bila ya shaka yoyotemtasikia udhia mwingi kutokana na walio pewa Kitabukabla yenu na wale walio shiriki. Na ikiwa mtasubirina mkamchamngu basi hakika hayo ni katika mambo yakuazimia.
[3.187] Na pale Mwenyezi Mungu alipo fungamana na waliopewa Kitabu kuwa: Lazima mtawabainishia watu, walahamtokificha, walikitupa nyuma ya migongo yao, na wakanunua kwacho thamani duni. Basi ni kiovu hichowalicho nunua.
[3.188] Usiwadhanie kabisa wale wanao furahia waliyoyafanya, na wakapenda kusifiwa kwa wasiyo yatenda,usiwadhanie kuwa watasalimika na adhabu. Yao wao niadhabu chungu.
[3.189] Na Ufalme wa mbingu na ardhi ni wa MwenyeziMungu; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye uweza juu ya kilakitu.
[3.190] Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi nakukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenyeakili,
[3.191] Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu wakiwa wima nawakikaa kitako na wakilala, na hufikiri kuumbwa mbinguna ardhi, wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi bure. Subhanaka, Umetakasika! Basi tukinge na adhabuya Moto.
[3.192] Mola wetu Mlezi! Hakika unaye mtia Motoniumemhizi; na walio dhulumu hawana wasaidizi.
[3.193] Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tumemsikia mwenyekuita akiitia Imani kwamba: Muaminini Mola wenu Mlezi;nasi tukaamini. Basi tusamehe madhambi yetu, na utufutie makosa yetu, na utufishe pamoja na watu wema.
[3.194] Mola wetu Mlezi! Na utupe uliyo tuahidi kwaMitume wako, wala usituhizi Siku ya Kiyama. HakikaWewe huvunji miadi.
[3.195] Mola Mlezi wao, akayakubali maombi yao akajibu:Hakika sipotezi kazi ya mfanya kazi miongoni mwenu,akiwa mwanamume au mwanamke, kwani ni nyinyi kwa nyinyi. Basi walio hama, na walio tolewa makwao, nawakateswa katika Njia yangu, na wakapigana, nawakauliwa, kwa yakini Mimi nitawafutia makosa yao, nakwa yakini nitawaingiza katika Mabustani yanayo pitamito kati yake. Hayo ndiyo malipo yanayo toka kwaMwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu kwake yapo malipomema kabisa.
[3.196] Kabisa kusikudanganye kubakia kutangatanga kwawalio kufuru katika nchi.
[3.197] Hiyo ni starehe ndogo. Kisha makaazi yao yatakuwaJahannamu. Na ni mahali pabaya mno pa kupumzikia.
[3.198] Lakini walio mcha Mola wao Mlezi watapataMabustani yanayo pita mito kati yake. Watadumu humo.Hayo ni makaribisho yao yatokayo kwa Mwenyezi Mungu.Na vilioko kwa Mwenyezi Mungu ni bora kwa watu wema.
[3.199] Hakika miongoni mwa Watu wa Kitabu wapo wanaomuamini Mwenyezi Mungu na yaliyo teremshwa kwenu nayaliyo teremshwa kwao, wakimnyenyekea Mwenyezi Mungu. Hawabadili Aya za Mwenyezi Mungu kwa thamani duni. Haowana ujira wao kwa Mola wao Mlezi. Hakika MwenyeziMungu ni Mwepesi wa kuhisabu.
[3.200] Enyi mlio amini! Subirini, na shindanenikusubiri, na kuweni macho, na mcheni Mwenyezi Mungu,ili mpate kufanikiwa.
Featured Ad
Home
About Us
What's New
Our Services
Search
Recommend This