Skip to Content
The Muslims Internet Directory
Featured Service
Home
|
Advertise
|
FAQ
|
Login/Register |
Directory
Quran
Hadith
Islamic Library
Prayer Times
Discover Islam
Islamic Gallery
Calendar
New
Classifieds
Services
Webmasters
Dictionary
Downloads
Kids & Games
Quran Navigation
Search
Translations
Transliteration
Index
Chapter Info
English Search
Articles and Books
Audio
Memorization
Links
Downloads
On Your Site
FAQ
Muslims Internet Directory
The Quran / English
The Hadith
2Muslims.com
Our Network
Islamic Library & Articles
The Internet
Islamic Classifieds
WebRing Members Sites
Advance
-
Live Search
-
Quran
-
Hadith
-
Search This Site
-
The Network
-
Classifieds
-
WebRing
-
The Internet
-
Help!
Featured Site
Feature Your Site Now
2Muslims Services
Islamic IE Toolbar
Islamic Internet Gadgets
Prayer Times Software
Forum
Donate
Islamic Quizzes
Islamic CGI Scripts
Polls
Free E-mail Account
Zakat Calculator
Islamic Holidays Dates
Islamic Date Converter
DAWA Tools
FAQ About Islam
Buy The Islamic CD
God's Attributes
How To Pray?
Paid Services
Buy The Islamic CD
Banner Design
Submit Your Site
Muslims Million Pixels
Translate Site To:
Arabic
Bulgarian
Catalan
Chinese (Simplified)
Chinese (Traditional)
Croatian
Czech
Danish
Dutch
English
Filipino
Finnish
French
German
Greek
Hebrew
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latvian
Lithuanian
Norwegian
Polish
Portuguese
Romanian
Russian
Serbian
Slovak
Slovenian
Spanish
Swedish
Ukrainian
Vietnamese
Hijab
Why do muslim females wear Hijab (Head cover)?
Faith
Culture
Fear
Other
view results
view other polls
Home
:
Quran:
Quran Translations:
Swahili:
SURAT AL- A'RAAF :
Search the Quran in any of the drop down menu languages:
--Select language--
Albanian
Arabic
Azerbaijani
Bengali
Bosnian
Brazilian
Burmese
Chinese
Dutch
English_Abdullah_Yusuufali
English_Hasan_Qaribullah
English_Muhammad_Pickthall
Farsi
Finish
French
German
Hausa
Hindi
Hindi
Indonesian
Italian
Japanese
Korean
Latin
Malaysian
Melayu
Meranao
Mexican
Pashto
Persian
Poland
Portuguese
Russian
Spanish
Swahili
Tamil
Thai
Transliteration
Turkish
Urdu
More search options
SURAT AL- A'RAAF
[7.1] ALIF LAM MYM 'SAAD
[7.2] Kitabu kilicho teremshwa kwako - basi isiwe dhikikifuani kwako kwa ajili yake, upate kuonya kwacho, nakiwe ni ukumbusho kwa Waumini.
[7.3] Fuateni mliyo teremshiwa kutoka kwa Mola Mleziwenu, wala msifuate rafiki au walinzi wengine badalayake. Ni machache mnayo yakumbuka.
[7.4] Na miji mingapi tuliiangamiza, ikaifikia adhabuyetu usiku au walipo kuwa wamelala adhuhuri.
[7.5] Basi hakikuwa kilio chao ilipo wafikia adhabu yetu,isipo kuwa kusema: Hakika sisi tulikuwa wenyekudhulumu.
[7.6] Na kwa yakini tutawauliza wale walio pelekewaUjumbe, na pia tutawauliza hao Wajumbe.
[7.7] Tena tutawasimulia kwa ilimu; wala Sisi hatukuwambali.
[7.8] Na Siku hiyo kipimo kitakuwa kwa Haki. Basi watakaokuwa na uzani mzito, hao ndio watakao fanikiwa.
[7.9] Na watakao kuwa na uzani khafifu, basi hao ndiowalio zitia khasarani nafsi zao kwa sababu yakuzipinga Ishara zetu.
[7.10] Na hakika tumekuwekeni katika ardhi, natumekujaalieni humo njia za kupatia maisha. Nikuchache kushukuru kwenu.
[7.11] Na hakika tulikuumbeni, kisha tukakutieni sura,kisha tukawaambia Malaika: Msujudieni Adam. Basiwakasujudu isipo kuwa Iblisi, hakuwa miongoni mwawalio sujudu.
[7.12] Mwenyezi Mungu akasema: Nini kilicho kuzuiakumsujudia nilipo kuamrisha? Akasema: Mimi ni borakuliko yeye. Umeniumba kwa moto, naye umemuumba kwa udongo.
[7.13] Akasema: Basi teremka kutoka humo! Haikufaliikufanya kiburi humo. Basi toka! Hakika wewe u miongonimwa walio duni.
[7.14] Akasema: Nipe muhula mpaka siku watakapo fufuliwa.
[7.15] Akasema: Utakuwa miongoni mwa walio pewa muhula.
[7.16] Akasema: Kwa kuwa umenihukumia upotofu, basinitawavizia katika Njia yako Iliyo Nyooka.
[7.17] Kisha nitawazukia mbele yao na nyuma yao nakuliani kwao na kushotoni kwao. Wala hutawakuta wengiwao wenye shukrani.
[7.18] Akasema: Toka humo, nawe umekwisha fedheheka,umekwisha fukuzwa. Hapana shaka atakaye kufuatamiongoni mwao, basi nitaijaza Jahannam kwa nyinyinyote.
[7.19] Na wewe, Adam! Kaa wewe na mkeo katika Bustanihii, na kuleni humo mpendapo. Wala msiukaribie mtihuu, mkawa katika wale walio dhulumu.
[7.20] Basi Shet'ani aliwatia wasiwasi ili kuwafichuliatupu zao walizo fichiwa, na akasema: Mola Mlezi wenuhakukukatazeni mti huu ila msije mkawa Malaika, au msije mkawa katika wanao ishi milele.
[7.21] Naye akawaapia: Kwa yakini mimi ni miongoni wawanao kunasihini.
[7.22] Basi akawateka kwa khadaa. Walipo uonja ule mti,tupu zao zilifichuka na wakaingia kujibandika majaniya Bustanini. Mola wao Mlezi akawaita: Je, sikukukatazeni mti huo, na kukwambieni ya kwambaShet'ani ni adui yenu wa dhaahiri?
[7.23] Wakasema: Mola wetu Mlezi! tumejidhulumu nafsizetu, na kama hutusamehe na kuturehemu, hakikatutakuwa katika wenye kukhasirika.
[7.24] Akasema: Teremkeni! Mtakuwa nyinyi kwa nyinyimaadui. Na kwenye ardhi itakuwa ndio makao yenu nastarehe yenu mpaka ufike muda.
[7.25] Akasema: Humo mtaishi, na humo mtakufa, na kutokahumo mtatolewa.
[7.26] Enyi wanaadamu! Tumekuteremshieni nguo za kufichatupu zenu, na nguo za pambo. Na nguo za uchamngu ndiobora. Hayo ni katika Ishara za Mwenyezi Mungu mpate kukumbuka.
[7.27] Eny wanaadamu! Asije Shet'ani kukufitinini kamaalivyo watoa wazazi wenu Peponi, akawavua nguo zaokuwaonyesha tupu zao. Hakika yeye na kabila yake wanakuoneni, na nyinyi hamuwaoni. Hakika Sisitumewafanya Mashet'ani kuwa ni marafiki wa wasioamini.
[7.28] Na wanapo fanya mambo machafu husema: Tumewakutanayo baba zetu, na Mwenyezi Mungu ametuamrisha hayo.Sema: Hakika Mwenyezi Mungu haamrishi mambo machafu. Mnamzulia Mwenyezi Mungu msiyo yajua?
[7.29] Sema: Mola Mlezi wangu ameamrisha uadilifu, namumuelekeze nyuso zenu kila mnapo sujudu, na muombeniYeye kwa kumsafia Dini. Kama alivyo kuumbeni mwanzo ndivyo mtavyo rudi,
[7.30] Hali ya kuwa kundi moja amelihidi, na kundijengine limethibitikiwa na upotofu. Kwa hakika haowaliwafanya mashet'ani kuwa ndio marafiki walinzibadala ya Mwenyezi Mungu, na wanadhani kuwa waowameongoka.
[7.31] Enyi wanaadamu! Chukueni pambo lenu kwenye kilapahala wakati wa ibada, na kuleni, na kunyweni na walamsifanye ubadhirifu. Kwa hakika Yeye hapendi wanao fanya israfu.
[7.32] Sema: Ni nani aliye harimisha pambo la MwenyeziMungu alilo watolea waja wake, na vilivyo vizurikatika riziki. Sema hivyo ni kwa walio amini katikauhai wa duniani, na Siku ya Kiyama vitakuwa vyao waotu. Namna hivi tunazieleza Ishara kwa watu wanao jua.
[7.33] Sema: Mola Mlezi wangu ameharimisha mambo machafuya dhaahiri na ya siri, na dhambi, na uasi bila yahaki, na kumshirikisha Mwenyezi Mungu na asichokiletea uthibitisho, na kumzulia Mwenyezi Mungu msiyoyajua.
[7.34] Na kila umma una muda wake. Utakapo fika muda waobasi hawatakawia hata saa moja, wala hawatatangulia.
[7.35] Enyi wanaadamu! Watakapo kufikieni Mitume miongonimwenu wakakuelezeni Ishara zangu, basi watakaomchamngu na wakatengenea haitakuwa khofu kwao, wala hawatahuzunika.
[7.36] Na wale watakao kanusha Ishara zetu nawakazifanyia kiburi, hao ni watu wa Motoni; humowatadumu.
[7.37] Basi ni nani dhaalimu mkubwa kuliko yule anayemzulia Mwenyezi Mungu uwongo, au anaye zikanushaIshara zake? Hao itawafikia sehemu yao waliyoandikiwa, mpaka watakapo wafikia wajumbe wetukuwafisha, watawaambia: Wako wapi mlio kuwa mkiwaomba badala ya Mwenyezi Mungu? Watasema:Wametupotea! Na watajishuhudia wenyewe kwamba walikuwamakafiri.
[7.38] Mwenyezi Mungu atasema: Ingieni Motoni pamoja naumma zilizo pita kabla yenu za majini na watu. Kilautakapo ingia umma utawalaani wenzake. Mpaka watakapo kusanyika wote humo, wa mwisho wao watawasema wamwanzo wao: Mola wetu Mlezi! Hawa ndio walio tupoteza;basi wape adhabu ya Motoni marudufu. Atasema: Itakuwa kwenu nyote marudufu, lakini nyinyi hamjui tu.
[7.39] Na wa mwanzo wao watawaambia wa mwisho wao: Basinyinyi pia hamkuwa na ubora kuliko sisi. Basi onjeniadhabu kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyachuma.
[7.40] Hakika wale wanao zikanusha Ishara zetu nawakazifanyia kiburi hawatafunguliwa milango ya mbingu,wala hawataingia Peponi mpaka apite ngamia katika tundu ya sindano. Na hivi ndivyo tunavyo walipawakosefu.
[7.41] Jahannamu itakuwa kitanda chao na juu yao nguo zamoto za kujifunika. Na hivi ndivyo tunavyo walipamadhaalimu.
[7.42] Na wale wanao amini na wakatenda mema -hatumkalifishi mtu yoyote ila kwa kiasi cha uwezo wake- hao ndio watu wa Peponi. Wao watadumu humo.
[7.43] Na tutaondoa chuki vifuani mwao, na mbele yao iweinapita mito. Na watasema: Alhamdulillah! Kuhimidiwani kwa Mwenyezi Mungu, ambaye aliye tuhidi kufikia haya. Wala hatukuwa wenye kuhidika wenyewe ingeli kuwaMwenyezi Mungu hakutuhidi. Hakika Mitume wa Mola wetuMlezi walileta Haki. Na watanadiwa kwamba: Hiyo ndiyoPepo mliyo rithishwa kwa sababu ya mliyo kuwamkiyafanya.
[7.44] Na watu wa Peponi watawanadia watu wa Motoni: Sisitumekuta aliyo tuahidi Mola wetu Mlezi kuwa ni kweli.Je, na nyinyi pia mmekuta aliyo kuahidini Mola wenu Mlezi kuwa ni kweli? Watasema: Ndiyo! Basimtangazaji atawatangazia: Laana ya Mwenyezi Munguiwapate walio dhulumu,
[7.45] Wale ambao walikuwa wakizuilia Njia ya MwenyeziMungu, na wakataka kuipotosha, nao wanaikanushaAkhera.
[7.46] Na baina ya makundi mawili hayo patakuwapo pazia.Na juu ya Mnyanyuko patakuwa watu watakao wajua wotekwa alama zao, na wao watawaita watu wa Peponi: Assalamu Alaykum, Amani juu yenu! Wao bado hawajaingiahumo, lakini wanatumai.
[7.47] Na yanapo geuzwa macho yao kuelekea watu waMotoni, watasema: Mola Mlezi wetu! Usitujaalie kuwapamoja na watu walio dhulumu.
[7.48] Na hao watu wa Mnyanyukoni watawaita watu wanaowajua kwa alama zao. Watasema: Kujumuika kwenuhakukufaini kitu, wala hicho mlicho kuwa mnafanyia kiburi.
[7.49] Je, hawa sio wale mlio kuwa mkiwaapia kuwaMwenyezi Mungu hatawafikishia rehema. Ingieni Peponi,hapana khofu kwenu, wala hamtahuzunika!
[7.50] Na watu wa Motoni watawaita watu wa Peponi:Tumimieni maji, au chochote alicho kuruzukuni MwenyeziMungu. Nao watasema: Hakika Mwenyezi Mungu ameviharimisha hivyo kwa makafiri,
[7.51] Ambao waliifanya dini yao kuwa ni pumbao namchezo, na maisha ya dunia yakawadanganya. Basi leoSisi tunawasahau kama walivyo usahau mkutano wa Siku yao hii, na kwa sababu ya kule kuzikataa Ishara zetu.
[7.52] Na hakika tumewaletea Kitabu tulicho kipambanuakwa ilimu, uwongofu na rehema kwa watu wenye kuamini.
[7.53] Je, lipo wanalo lingojea isipo kuwa matokeo yake?Siku yatapo fika matokeo yake watasema wale waliokisahau: Kweli Mitume wa Mola Mlezi wetu waliletaHaki! Je, tunao waombezi ili watuombee? Au turudishweili tufanye yasiyo kuwa yale tuliyo kuwa tukiyafanya?Bila ya shaka wamejikhasiri nafsi zao, na yamewapotea waliyo kuwa wakiyazua.
[7.54] Hakika Mola Mlezi wenu ni Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kishaakatawala juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwamchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, nanyota zinazo tumika kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba naamri ni zake. Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, MolaMlezi wa viumbe vyote.
[7.55] Muombeni Mola wenu Mlezi kwa unyenyekevu na kwasiri. Hakika Yeye hawapendi warukao mipaka.
[7.56] Wala msifanye uharibifu katika nchi baada ya kuwaimekwisha tengenezwa. Na muombeni kwa kuogopa na kwakutumai. Hakika rehema ya Mwenyzi Mungu iko karibu na wanao fanya mema.
[7.57] Na Yeye ndiye anaye peleka pepo (za kuvuma) kuwani bishara kabla ya kufika rehema yake. Hata hizo pepozinapo beba mawingu mazito tunayachunga mpaka kwenye nchi iliyo kufa. Kisha tunateremsha kwayo maji, ndiokama hivyo tukatolesha kila aina ya matunda. Basi halikadhaalika tunavyo wafufua wafu, ili mpate kukumbuka.
[7.58] Na ardhi njema, yenye udongo wa rutba, hutoa mimeayenye kukua vizuri yenye uhai, kwa idhini ya MolaMlezi wake. Na ardhi mbaya haitoi ila mimea michache, isiyo na faida, tena kwa shida. Na hivyo ndivyotunavyo zipambanua Ishara (Aya) kwa watu wanaoshukuru.
[7.59] Tulimpeleka Nuhu kwa kaumu yake, naye akasema:Enyi kaumu yangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyihamna Mungu ila Yeye. Hakika mimi ninakukhofieniadhabu ya Siku iliyo kuu.
[7.60] Wale watukufu katika kaumu yake wakasema: Hakikasisi tunakuona wewe umo katika upotofu ulio dhaahiri.
[7.61] Akasema: Enyi watu wangu! Mimi simo katikaupotofu, lakini mimi ni Mtume nitokaye kwa Mola Mleziwa viumbe vyote.
[7.62] Nakufikishieni Ujumbe wa Mola Mlezi wangu, naninakunasihini; na ninayajua kwa Mwenyezi Mungu msiyoyajua nyinyi.
[7.63] Je, mnastaajabu kukujieni mawaidha yanayotoka kwaMola Mlezi wenu kwa njia ya mtu aliye ni mmoja katikanyinyi, ili akuonyeni na ili mumchemngu, na ili mpate kurehemewa?
[7.64] Basi walimkanusha. Nasi tukamwokoa yeye na waliokuwa pamoja naye katika jahazi. Na tukawazamisha walewalio kanusha Ishara zetu. Hakika hao walikuwa watu vipofu.
[7.65] Na kwa A'adi tulimpeleka ndugu yao, Hud. Akasema:Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyihamna mungu ila Yeye. Basi je, hamumchi?
[7.66] Wakasema watukufu wa wale walio kufuru katikakaumu yake: Sisi tunakuona umo katika upumbavu, nahakika sisi tunakufikiria kuwa wewe ni katika waongo.
[7.67] Akasema: Enyi watu wangu! Mimi sina upumbavu.Lakini mimi ni Mtume niliye toka kwa Mola Mlezi waviumbe vyote.
[7.68] Nakufikishieni ujumbe wa Mola wangu Mlezi. Na mimikwenu ni mwenye kukunasihini, muaminifu.
[7.69] Mnaona ajabu kukufikieni mawaidha yanayo toka kwaMola wenu Mlezi kwa mtu aliye mmoja wenu nyinyi iliakuonyeni? Na kumbukeni alivyo kufanyeni mshike pahala pa kaumu ya Nuhu, na akakuzidisheni katikaumbo. Basi zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu ilimpate kufanikiwa.
[7.70] Wakasema: Je! Umetujia ili tumuabudu MwenyeziMungu peke yake, na tuyaache waliyo kuwa wakiyaabudubaba zetu? Basi tuletee hayo unayo tuahidi, ukiwa miongoni mwa wasemao kweli.
[7.71] Akasema: Bila ya shaka adhabu na ghadhabuzimekwisha kukuangukieni kutoka kwa Mola wenu Mlezi.Mnabishana nami kwa ajili ya majina tu mliyo yaitanyinyi na baba zenu ambayo kwayo Mwenyezi Munguhakuteremsha uthibitisho? Basi ngojeni, mimi pia ni pamoja nanyi katika wanao ngoja.
[7.72] Basi tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye kwarehema zetu, na tukakata mizizi ya wale waliozikanusha Ishara zetu, na hawakuwa wenye kuamini.
[7.73] Na kwa Thamud tulimpeleka ndugu yao, Saleh.Akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu.Nyinyi hamna Mungu ila Yeye. Hakika imekwisha kukufikieni Ishara iliyo wazi kutoka kwa Mola wenuMlezi. Huyu ni ngamia jike wa Mwenyezi Mungu aliye niIshara kwenu. Basi mwachieni ale kwenye ardhi ya Mwenyezi Mungu, wala msimdhuru, isije kukushukieniadhabu chungu.
[7.74] Na kumbukeni alivyo kufanyeni wa kushika pahala paA'adi na akakuwekeni vizuri katika nchi, mnajengamajumba ya fakhari katika nyanda zake, na mnachonga majumba katika milima. Basi zikumbukeni neema zaMwenyezi Mungu wala msitende uovu katika nchi kwaufisadi.
[7.75] Waheshimiwa wa kaumu yake wanao jivuna waliwaambiawanao onewa wenye kuamini miongoni mwao: Je,mnaitakidi ya kwamba Saleh ametumwa na Mola Mleziwake? Wakasema: Hakika sisi tunayaamini yale aliyotumwa.
[7.76] Wakasema wale wanao jivuna: Sisi tunayakataa hayomnayo yaamini.
[7.77] Na wakamuuwa yule ngamia, na wakaasi amri ya MolaMlezi wao, na wakasema: Ewe Saleh! Tuletee unayotuahidi ikiwa wewe ni miongoni mwa Mitume.
[7.78] Basi tetemeko la ardhi likawanyakua, na kulipokucha wakawa majumbani mwao kifudifudi wamekwishakufa.
[7.79] Basi Saleh akwaacha na akasema: Enyi watu wangu!Nilikufikishieni Ujumbe wa Mola wangu Mlezi, nanikakunasihini, lakini nyinyi hamwapendi wenye nasaha.
[7.80] Na tulimtuma Lut', alipo waambia watu wake: Je,mnafanya uchafu ambao hajakutangulieni yeyote kwauchafu huo katika viumbe vyote!
[7.81] Hivyo nyinyi mnawaingilia wanaume kwa matamaniomkwawacha wanawake? Kumbe nyinyi ni watu wafujaji!
[7.82] Na haikuwa jawabu ya kaumu yake isipo kuwakuambizana: Wafukuzeni katika mji wenu, maana hao niwatu wanao jitakasa.
[7.83] Basi tukamwokoa yeye na watu wake, isipo kuwamkewe, alikuwa miongoni mwa walio bakia nyuma.
[7.84] Na tukawamiminia mvua. Basi tazama jinsi ulivyokuwa mwisho wa wakosefu.
[7.85] Na kwa watu wa Madyana tulimtuma ndugu yaoShua'ib. Akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni MwenyeziMungu. Hamna mungu mwengine isipo kuwa Yeye. Imekwishakufikieni hoja wazi kutoka kwa Mola Mlezi wenu. Basitimizeni sawasawa vipimo na mizani, wala msiwapunjewatu vitu vyao, wala msifanye uharibifu katika nchi, baada ya kuwa imekwisha tengenea. Hivi ndivyo borakwenu ikiwa nyinyi ni Waumini.
[7.86] Wala msikae katika kila njia mkitisha watu, nakuwazuilia na Njia ya Mwenyezi Mungu wale wenyekumuamini, na mkataka njia ipotoke. Na kumbukeni mlipokuwa wachache, naye akakufanyeni kuwa wengi. Natazameni jinsi ulivyo kuwa mwisho wa mafisadi.
[7.87] Na kama liko kundi miongoni mwenu lililo aminihaya niliyo tumwa, na kundi jengine halikuamini, basisubirini mpaka Mwenyezi Mungu ahukumu baina yetu. Nayendiye Mbora wa wenye kuhukumu.
[7.88] WAHESHIMIWA WALIO TAKABARI katika kaumu yakewakasema: Ewe Shua'ib! Tutakutoa wewe pamoja na walewalio kuamini katika mji wetu, au mrejee katika mila yetu. Akasema: Je, ingawa tunaichukia?
[7.89] Bila ya shaka itakuwa tumemzulia uwongo MwenyeziMungu tukirudi katika mila yenu baada ya kwisha tuokoanayo Mwenyezi Mungu. Wala haiwi kwetu sisi kuirejea mila hiyo, ila akitaka Mwenyezi Mungu, Mola Mleziwetu. Ujuzi wa Mola Mlezi wetu umeenea katika kilakitu. Kwa Mwenyezi Mungu tunategemea. Ewe Mola Mleziwetu! Tuhukumie baina yetu na kaumu yetu kwa haki,nawe ndiye mbora wa wanao hukumu.
[7.90] Na waheshimiwa walio kufuru katika kaumu yakewakasema: Mkimfuata Shua'ib, basi hakika hapo nyinyimtakuwa mlio khasiri.
[7.91] Basi tetemeko la ardhi likawanyakua, na wakaamkiamajumbani mwao wamejifudikiza, wamekwisha kufa.
[7.92] Wale walio mkanusha Shua'ib wakawa kama kwambahawakuwako. Walio mkanusha Shua'ib ndio walio kuwawenye kukhasiri.
[7.93] Basi akawaachilia mbali na akasema: Enyi kaumuyangu! Nimekufikishieni Ujumbe wa Mola Mlezi wangu, nanimekunasihini; basi vipi niwahuzunikie watu makafiri?
[7.94] Na hatukumtuma Nabii yeyote katika mji ilatuliwapatiliza wakaazi wake kwa taabu na mashaka iliwapate kunyenyekea.
[7.95] Kisha Sisi hubadilisha mahala pa ubaya kwa wema,hata wakazidi, na wakasema: Taabu na raha ziliwafikiababa zetu. Basi kwa ghafla tukawashika, hali ya kuwa hawajatambua.
[7.96] Na lau kuwa watu wa miji wangeli amini nawakamchamngu, kwa yakini tungeli wafungulia barakakutoka mbinguni na katika ardhi. Lakini walikanushabasi tukawapatiliza kwa sababu ya yale waliyo kuwawakiyachuma.
[7.97] Je, watu wa mijini wameaminisha ya kuwa adhabuyetu haitawafika usiku, nao wamelala?
[7.98] Au watu wa mijini wameaminisha ya kuwa adhabu yetuhaitawafika mchana, nao wanacheza?
[7.99] Je, wamejiaminisha na mipango ya Mwenyezi Mungu?Kwani hawajiaminishi na mipango ya Mwenyezi Mungu ilawatu wenye kukhasiri.
[7.100] Je, hawahidiki hawa wanao rithi ardhi baada yawale wenyewe kwamba tukitaka tutawapatiliza kwamadhambi yao, na tutapiga muhuri juu ya nyoyo zao, nakwa hivyo hawatasikia?
[7.101] Miji hiyo, tunakusimulia baadhi ya khabari zake.Na hapana shaka Mitume wao waliwafikia kwa hoja zilizowaziwazi. Lakini hawakuwa wenye kuamini waliyo yakanusha zamani. Namna hivi Mwenyezi Mungu anazipigamuhuri nyoyo za makafiri.
[7.102] Wala hatukuwaona wengi wao kuwa wanatimiza ahadi;bali kwa hakika tuliwakuta wengi wao ni wapotofu.
[7.103] Kisha baada yao tukamtuma Musa na Ishara zetu kwaFirauni na waheshimiwa wake. Nao wakazikataa. Basitazama ulikuwaje mwisho wa waharibifu.
[7.104] Na Musa alisema: Ewe Firauni! Hakika mimi niMtume nitokaye kwa Mola Mlezi wa viumbe vyote.
[7.105] Inafaa nisiseme juu ya Mwenyezi Mungu ila liliola Haki. Nami hakika nimekujieni na dalili waziwazikutokana na Mola Mlezi wenu. Basi waache Wana wa Israili wende nami.
[7.106] Akasema Firauni: Ikiwa umekuja na Ishara, basiilete ukiwa ni katika wasemao kweli.
[7.107] Basi akaitupa fimbo yake, na mara ikawa nyokadhaahiri.
[7.108] Na akatoa mkono wake, mara ukawa mweupe kwawatazamao.
[7.109] Wakasema waheshimiwa wa kaumu ya Firauni: Hakikahuyo ni mchawi mjuzi.
[7.110] Anataka kukutoeni katika nchi yenu. Basi mnatoashauri gani?
[7.111] Wakasema: Mwache kidogo yeye na nduguye, nawatume mijini wakusanyao,
[7.112] Wakuletee kila mchawi mjuzi.
[7.113] Wakaja wachawi kwa Firauni, wakasema: Hakikatutapata ujira ikiwa tutashinda.
[7.114] Akasema: Naam! Nanyi bila ya shaka mtakuwa katikawa karibu nami.
[7.115] Wakasema: Ewe Musa! Je, utatupa wewe, au tutakuwasisi tutao tupa?
[7.116] Akasema: Tupeni! Basi walipo tupa waliyazugamacho ya watu na wakawatia khofu, na wakaleta uchawimkubwa.
[7.117] Nasi tukamfunulia Musa kumwambia: Tupa fimboyako. Mara ikavimeza vyote vile walivyo vibuni.
[7.118] Kweli ikathibiti na yakabat'ilika waliyo kuwawakiyatenda.
[7.119] Kwa hivyo walishindwa hapo, na wakageuka kuwawadogo.
[7.120] Na wachawi wakapoomoka wakisujudu.
[7.121] Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa viumbe vyote,
[7.122] Mola Mlezi wa Musa na Haarun.
[7.123] Akasema Firauni: Mmemuamini kabla sijakupeniidhini? Hizi ni njama mlizo panga mjini mpate kuwatoawenyewe. Lakini karibu mtajua!
[7.124] Lazima nitaikata mikono yenu na miguu yenu mbalimbali. Kisha nitakutundikeni misalabani.
[7.125] Wakasema: Sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetuMlezi.